October 26, 2015

  • Vibanda vya Mama Lishe na Mitumba Vyachomwa Moto Mkoani Njombe....Polisi Yawataka Wananchi Kuwa Watulivu Wakati Wakisubiri Matokeo



    Vibanda vya Mama Lishe na Mitumba Vyachomwa Moto Mkoani Njombe....Polisi Yawataka Wananchi Kuwa Watulivu Wakati Wakisubiri Matokeo

    Moto ambao chanzo chake hakijajulikana hadi sasa umeteketeza baadhi ya mabanda ya mama lishe na mitumba karibu na kituo cha mabasi mkoani Njombe.

    Hata hivyo, kikosi cha Zimamoto mkoani humo kimefanikiwa kuuzima moto huo usiku wa kuamkia leo ambapo polisi wamesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

    Kwa mujibu kikosi hicho, mabanda mengine yamesalimika katika ajali hiyo.

    Hata hivyo, kikosi hicho kimewataka wananchi kuwa watulivu wakati huu wakisubiri matokeo ya uchaguzi ambayo yanatarajiwa kutolewa muda wowote mkoani humo.

    Kwa mujibu wa kituo cha luninga cha AzamTV, polisi mkoani humo wamesema uchaguzi mkoani humo ulifanyika kwa utulivu na hsata moto huo ulipotokea, wananchi wengi walikuwa majumbani mwao.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.