October 27, 2015

  • CCM Wailalamikia tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC)



    CCM Wailalamikia tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC)
    Na Mhamed khamis Zanzibar. 

    Chama cha Mapinduzi CCM Zanzibar kimesema hakina imani na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) katika uendeshaji nzima wa uchaguzi. 

    Akizungumza na waandishi wa habari visiwani hapa Naibu katibu mkuu CCM Bwana Vua Ali Vuai amesema baadhi ya maeneo mawakala wa Chama chao walinyimwa vitamulisho jambo ambalo limekifanya chama hicho kutokuridhika na utaratibu huo. 

    Amesema siku moja kabla ya uchaguzi walifika tume ya uchaguzi kuhakiki vitambulisho vya mawakala wao wote na vilikuwepo. 

    Amesema cha kushangaza ni kuwa siku ya kura vitambulisho vya mawakala hao havikuonekana wala hakujulikana nani alivichukua

    "Kutokana na hali hii tunakosa imani na ZEC " alisema Vuai.
    ANGALIA VIDEO HAPA:


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.