JUKWAA la Wahariri Nchini (TEF), limewataka wanahabari kuwa makini na maisha yao wakati huu wa mchakato wa uchaguzi sambamba na kulaani kitendo cha vijana wa Chadema cha kumshambulia na kumpiga mwandishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Christopher Lissa.
Aidha,                limewataka vyama vya siasa na watu binafsi wanaoandaa                mikutano ya waandishi wa habari kutowaalika makada wa                vyama vyao ambao si wanataaluma katika mikutano hiyo.
        Akizungumza                jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa TEF, Absalom                Kibanda alisema kitendo cha kumpiga mwandishi wa habari                hakivumiliki, kwani ni sawa na kuipiga na kushambulia                taaluma nzima ya wanahabari.
        Alisema                tukio la kupigwa Lissa ni mwendelezo wa vitendo vyenye                mwelekeo wa kuwazuia waandishi wa habari kutekeleza wajibu                wao wa msingi wa kukusanya taarifa na kuuhabarisha umma wa                Watanzania.
        âIfahamike                  kuwa vitendo vya watu kuwashambulia waandishi wa habari                  wakiwa kazini siyo tu vinakwaza utendaji wao wa kazi,                  bali vinadhalilisha utu wao mbele wa jamii                  inayowazunguka."
        Kibanda                alisema huu ni wakati wa waandishi wa habari kuchukua                tahadhari wakati wakiripoti matukio ambayo yanaweza                kusababisha vurugu na madhara kwao na kwa vitendea kazi                kama kamera, magari.
        â                  Hakuna habari yenye thamani zaidi ya maisha yako                  mwandishi wa habari,â alisisitiza.
              
Kibanda amevitaka vyama vya siasa kama taasisi, viongozi, wanachama na wapenzi wa vyama hivyo, kuacha mara moja vitendo vya kuwashambulia waandishi wa habari kwa sababu zozote zile na kama vitendo hivyo vitaendelea hawatasita kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kususia matukio na mikutano yao.
        Kibanda amevitaka vyama vya siasa kama taasisi, viongozi, wanachama na wapenzi wa vyama hivyo, kuacha mara moja vitendo vya kuwashambulia waandishi wa habari kwa sababu zozote zile na kama vitendo hivyo vitaendelea hawatasita kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kususia matukio na mikutano yao.
â                  Tukiona vitendo hivi vinaendelea TEF kwa kushirikiana na                  taasisi nyingine za kihabari haitasita kuchukua hatua                  zaidi dhidi ya vyama husika na ikibidi, kususia matukio                  na mikutano ya vyama hivyo.
        "Hatutaki                  kuona waandishi wa habari wanakuwa punching box kwani                  urafiki wa mwandishi wa habari na mwanasiasa au mchumi                  ni wa kitaaluma, hivyo hatutamvumilia mtu awaye yeyote                  atakayeingilia msingi wa wanataaluma ya habari ,â alisema.
        Akihojiwa                juu ya taarifa hiyo ya TEF, kwa njia ya simu jana, Ofisa                Habari wa Chadema, Tumaini Makene alisema hawezi kujibu                kwa simu kuhusu walichokisema wahariri na kudai apewe muda                wa kupitia taarifa hiyo ili atoe jibu lenye uhakika.
        Mwishoni                mwa wiki, Mwandishi wa UPL, Lissa alipigwa na vijana wa                Chadema kwenye makao makuu ya chama hicho wakati mwandishi                huyo alipokwenda kupiga picha maandamano ya vijana                waliopinga kuondoka kwa katibu wa chama hicho Dk Willbrod                Slaa.
        
0 comments:
Post a Comment