Dar es Salaam.                Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Twaweza, umebaini kuwa                sera ndiyo kigezo muhimu watakachokitumia wananchi                kumchagua Rais katika Uchaguzi Mkuu.
            Akitoa matokeo ya                  utafiti huo jana, Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa                  Twaweza, Aidan Eyakuze alisema asilimia 46 ya wananchi                  walisema watamchagua Rais kwa sera zake nzuri huku                  asilimia 17 wakisema kwa maadili na uadilifu wake.
            Akifafanua, alisema                utafiti huo wenye jina la 'Je wajua takwimu kuhusu uelewa                wa wapiga kura', uliwahoji wananchi 1,335 wa Tanzania                Bara. Vigezo vingine na asilimia katika mabano ni utajiri                (0) uzoefu wa kisiasa (11), uzoefu wa kitaaluma (3) na                ukabila (3).
            Eyakuze alisema ingawa                kwenye majukwaa ya kisiasa wagombea wa urais wanapigana                vijembe, matokeo ya utafiti huo yanaonyesha kuwa wananchi                wanahitaji zaidi sera ili kumpata Rais bora ajaye.
            Alisema wananchi 82                wanaamini kwamba Uchaguzi Mkuu utakuwa huru na uamuzi wao                utaheshimika.
            Alisema asilimia 54 ya                watu waliohojiwa wana wasiwasi wa kutokea machafuko ingawa                Twaweza haikukusanya takwimu za nani anaweza kuwa chanzo                cha vurugu.
            Kuhusu Sheria ya                Uchaguzi, Eyakuze alisema asilimia 75 ya walisema                wanafahamu kuwa wagombea hawaruhusiwi kugawa fedha kwa                wapiga kura ili wawachague, wakati asilimia 25 hawajui.
            Pia, asilimia 76 walisema                wanaamini vyombo vya habari vitaripoti kwa usahihi masuala                yanayohusu uchaguzi mkuu.
            wakati asilimia 24                walisema vitakuwa na upendeleo kwa sababu ya kupatiwa                motisha na fedha.
          
0 comments:
Post a Comment