WAHADHIRI takriban 800 waliopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) wameazimia kutoingia madarasani kufundisha kuanzia Novemba 2 mwaka huu mpaka hapo serikali itakaposhughulikia suala la muundo mpya wa mishahara.
Kauli                hiyo ilitolewa jana na Kaimu Mwenyekiti wa Umoja wa                Wanataaluma wa UDOM (Udomasa), Gerald Shija alipokuwa                akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maazimio ya                mkutano mkuu wa wanataaluma hao uliofanyika Septemba 21                mwaka huu.
                Amesema                kwa pamoja wameazimia na kutoa msimamo huo mpaka hapo                serikali itakapotekeleza.
                Kwa                mujibu wa Shija alidai kuwa Rais alitoa taarifa kupitia                vyombo vya habari Agosti 22 mwaka 2013 ambao uliagiza                muundo huo uanze kutumika Julai Mosi mwaka huu lakini                mpaka sasa haujaanza.
                Amesema                kumekuwepo na mishahara isiyofanana kwa watu wenye elimu                inayofanana na kufanya kazi inayofanana na hivyo                kutofautiana na sera ya Serikali inayoelekeza kuwa watu                wenye elimu inayofanana kulipwa mishahara inayofanana.
                Shija                amesema wanaamini kuwa muundo huo wa utumishi ulioanishwa                na wanataaluma ndio muundo bora ukilinganisha na muundo                unaotumika sasa hivi.
                Aliiomba                serikali kutekeleza muundo huo ili kuondoa kero ambazo                zilibainishwa kwa Rais, hali iliyomfanya aagize                uanzishwaji na utekelezwaji wa muundo huo.
                Aidha                amesema hivi sasa hawana imani na viongozi wa serikali                kutokana na kutotekeleza muundo huo katika kutatua kero za                muundo uliopo hivi sasa.
                "Ucheweleshwaji                  wa muundo huu umekuwa ukikwamishwa na Hazina, Chuo Kikuu                  cha Dodoma pamoja na Utumishi wa umma ambapo wamekuwa                  wakitupiana mpira," amesema Shija.
                Hata                hivyo amesema mnamo Desemba 11, 2014, Ofisi ya Msajili wa                Hazina ilitoa waraka kuagiza Vyuo kupitia Ofisi za                rasilimali watu kuzingatia utaratibu ulioanishwa katika                muundo na wanataaluma ikiwemo masuala ya vyeo na kuajiri                kwakuzingatia vigezo na kuwapanga watumishi wanataaluma.
                Naye                Katibu Mkuu wa Umoja huo, Lameck Thomas amesema kuwa                muundo huo ulilenga kuweka usawa wa maslahi ya watendaji                wa Vyuo vikuu na Vyuo vya Umma na vyuo vikuu vishiriki ili                wawe sawa lakini hakuna kilichotekelezwa.
                "Kwa                  kweli nieleze kwa masikitiko makubwa na tusingependa                  tufikie hatua hii lakini serikali ndio imetufanya                  tufikie hapa, tutahakikisha tunapigania muundo huu hadi                  tupate haki zetu kwani ni nyenzo sahihi lakini tatizo la                  kulipwa mishahara tofauti kwa wahadhiri lipo katika Chuo                  Kikuu cha Dodoma tofauti na vyuo vingine," amesema                Thomas.
                Kwa                upande wake, Mjumbe wa Kamati Utendaji ya Udomasa, Mandela                Peter amesema bora muundo huo uje ili kuleta usawa                kutokana na kutofautiana kwa kiasi kikubwa mishahara kwa                wahadhiri wa UDOM na vyuo vingine kama vile Chuo kikuu cha                Dar es salaam (UDSM).
                "Yaani                  ukiangalia katika vyuo vya UDSM, Sokoine, Mzumbe                  ukilinganisha na UDOM kuna tofauti kubwa kati ya Sh.                  700,000 hadi 1,000,000 kwa mshahara anaopokea mhadhiri                  msaidizi, sasa hapo utaona kutokana na tofauti hiyo ni                  bora muundo huu uanze kutekelezwa ili tuwe sawa,"                amesema Mandela.
                Aidha                Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya                Juu Tanzania (THTU) katika chuo hicho, Nashon Maisori                aliiomba serikali kutopuuza madai hao kwani wasipoyapatia                ufumbuzi watasababisha zaidi ya wanafunzi 18,000                kuathirika kutokana na hali hiyo.
         
0 comments:
Post a Comment