September 29, 2015

  • JAJI LUBUVA ASEMA MADAI YA MBOWE HAYANA UKWELI


    JAJI LUBUVA ASEMA MADAI YA MBOWE HAYANA UKWELI
    Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekanusha tuhuma kuwa baadhi ya wakurugenzi wa NEC wameachishwa kazi ghafla na kazi zao wamepewa watu ambao watakipendelea Chama cha Mapinduzi.

    Mwenyekiti wa Tume Jaji Lubuva amesema tuhuma zilizoibuliwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe hazina ukweli wowote na zinapotosha Umma.
    Mbowe alisema kuwa maafisa wa Usalama wa Taifa wamepewa nafasi za uongozi ndani ya NEC
    Jaji Lubuva amesema kuwa kuna mabadiliko yalifanyika mwezi uliopita ambapo Rais Kikwete alimteua Julius Malaba kuwa Mkurugenzi mpya wa Uchaguzi kwa lengo la kuimarisha utendaji wa Tume na sio vinginevyo.
    Jaji Lubuva ameomba baadhi ya viongozi wa kisiasa kuacha kuipotosha jamii


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.