
Mwenyekiti wa Tume Jaji Lubuva amesema tuhuma zilizoibuliwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe hazina ukweli wowote na zinapotosha Umma.
Mbowe alisema kuwa maafisa wa Usalama wa Taifa wamepewa nafasi za uongozi ndani ya NEC
Jaji Lubuva amesema kuwa kuna mabadiliko yalifanyika mwezi uliopita ambapo Rais Kikwete alimteua Julius Malaba kuwa Mkurugenzi mpya wa Uchaguzi kwa lengo la kuimarisha utendaji wa Tume na sio vinginevyo.
Jaji Lubuva ameomba baadhi ya viongozi wa kisiasa kuacha kuipotosha jamii
0 comments:
Post a Comment