Miaka            130 iliyopita,  ulifanyika mkutano wa Berlin ambao ndiyo            ulikuwa mwanzo wa ukoloni barani Afrika, ulimalizika. Ni            Katika mkutano huo ambapo wakoloni waliweka mipaka ya makoloni            yao barani Afrika.
          
          
          
        Tarehe            26 Februari mwaka 1885 ilikuwa siku ya mwisho ya mkutano wa            Berlin ambao ulileta mabadiliko ya kudumu barani Afrika.            Wawakilishi wa nchi 13 za Ulaya na wengine kutoka Marekani            walikutana kwenye ofisi ya Kansela wa Ujerumani Berlin kugawa            maeneo ya bara la Afrika.
        Katika            chumba cha mkutano palikuwa na ramani ya Afrika yenye urefu wa            mita tano. Ilionyesha milima, maziwa na mito mbali mbali            iliko. Ni mkutano uliokuwa umeitishwa na Kansela Otto von            Bismarck na lengo lilikuwa kuwapa wakoloni maeneo ya kutawala.            Hata hivyo hakuna hata mwakilishi mmoja wa Afrka aliyealikwa            kwenye mkutano huo. Miaka michache baada ya mkutano huu nchi            zote za kiafrika, isipokuwa tu Ethiopia na Liberia, zilikuwa            chini ya utawala wa kikoloni.
        Profesa            wa historia katika chuo kikuu cha Nasarawa nchini Nigeria            Olayemi Akinwumi, anasema katika mkutano huo maeneo yaligawiwa            kiholela, na hilo limekuwa na athari zake hadi leo.
        "Sisi            watafiti wa masuala ya Afrika, wengi wetu tunaamini kuwa            chanzo cha migogoro mingi inayoendelea Afrika kwa wakati huu            ni mkutano wa Berlin wa mwaka 1884/1885. Waliligawa bara la            Afrika bila kujali historia ya jamii zilizokuwepo." Amesema            Akinwumi.
        Jamii            zilitenganishwa
        Kwa            sababu hiyo, hata makabila yalitenganishwa na hivyo sehemu ya            watu wa jamii moja kuwa kwenye nchi fulani huku wenzao            wakijikuta nchi nyingine. Hata njia za biashara zilikatishwa            kwa kuwa haikuruhusiwa tena kufanya biashara na watu wa koloni            jingine. Utafiti unaonyesha kwamba maeneo ambapo jamii            zilitengwa kwa mipaka ya nchi yanashuhudia migogoro mingi            zaidi.
        Katika            miaka ya 1960 nchi nyingi za Afrika zilipata uhuru na hivyo            kulikuwa na fursa ya kufuta mipaka ya nchi iliyowekwa na            wakoloni. Lakini kama anavyosema mtafiti wa Historia ya Afrika            katika chuo kikuu cha Dresden nchini Ujerumani, Michael Pesek.
        'Idadi            kubwa ya wanasiasa wa Kiafrika mwaka 1960 walisema, "mkifanya            hivyo mtakuwa mnaanzisha balaa". Ni kweli kwamba katika miaka            80 iliyopita Afrika imeshuhudia migogoro mingi baina ya nchi            na nchi lakini ni mara chache kabisa migogoro hiyo ilihusiana            na masuala ya mipaka", amesema mtafiti huyo.
        Fidia            kwa Afrika ni kama ndoto
        Mwaka            2010, miaka 125 baada ya mkutano wa Berlin, wawakilishi wa            nchi Kiafrika walikwenda Berlin kudai kulipwa fidia na kuombwa            msamaha kwa sababu ya athari za ukoloni kwa nchi zao. Katika            tamko lao waliutaja uamuzi wa kuigawanya Afrika bila            kuzingatia sheria wala utamaduni wa Kiafrika kuwa ni uhalifu            dhidi ya ubinadamu. Lakini hakuna chochote kilichotokea.
        Mtafiti            Michael Pesek ameendelea kusema, "Tunazungumza sana kuhusu            fidia kwa ajili ya biashara ya watumwa ama mauaji ya Wayahudi.            Lakini ni mara chache utasikia wakizungumzia uhalifu            uliofanywa na Wakoloni walipokuwa barani Afrika kwa zaidi ya            miaka 100,"
        Naye            Olayemi Akinwumi kutoka Nigeria amekubaliana na maoni hayo ya            mwenzake wa Ujerumani, akisema haamini kama utakuja kuwepo            muda wa kufikiria aina yoyote ya fidia kwa Afrika.
        Ni            muhimu kuashiria kwamba, wanaafrika wanatakiwa wawe na uchungu            wa kukumbuka matukio ya zamani na kujifunza kupitia matukio            hayo, inawapasa kufahamu na kukumbuka dhulma, uadui, na            uhalifu uliyofanywa na wakoloni dhidi yao, wanapaswa            wajitegemee badala ya kuwategemea watu waliowadhulumu na            kuwanyanyasa.
        TAFAKURI.COM
        
0 comments:
Post a Comment