Mkitaka            kujua afya yangu, mimi ni mzima wa afya. Namshukuru Mungu            naendelea vizuri na majukumu yangu ya kila siku likiwemo hili            la kuwaandikia barua watu mbalimbali maarufu na wasio            maarufu.Leo nimeona niwaandikie Watanzania wote kwa ujumla            maana nimeguswa na hali ya kisiasa inayoendelea nchini, siasa            ndiyo kila kitu kwa sasa.
        Dhumuni la            kuwaandikia barua hii ni kutaka kuwakumbusha kwamba katika            kipindi hiki cha uchaguzi, tunapaswa kutofautiana kiitikadi            lakini tuepuke mihemuko iliyopitiliza kiasi cha kuanza            kutukanana 'live' au mitandaoni.
Ndugu zangu, uchaguzi utapita Oktoba 25, mwaka huu. Maisha yataendelea kama kawaida. Maendeleo ya mtu mmojammoja mbali na kuwezeshwa na serikali kwa namna moja au nyingine, lakini jitihada binafsi zinahitajika ili uweze kupiga hatua.
        Ndugu zangu, uchaguzi utapita Oktoba 25, mwaka huu. Maisha yataendelea kama kawaida. Maendeleo ya mtu mmojammoja mbali na kuwezeshwa na serikali kwa namna moja au nyingine, lakini jitihada binafsi zinahitajika ili uweze kupiga hatua.
Hakuna            kiongozi atakayekuletea mafanikio wakati wewe hujishughulishi.            Kilichonisukuma zaidi kuwaandikia barua hii, nafahamu juu ya            matusi, kejeli ambazo mmekuwa mkizifanya katika mitandao ya            kijamii na hata mnapokuwa vijiweni.
Tunachafuana, tunawachafua viongozi wetu tena wakati mwingine hawana kosa lolote. Tunatengeneza chuki. Chuki hii itatugharimu sasa na hata baada ya uchaguzi. Tuwe makini sana kipindi hiki.
        Tunachafuana, tunawachafua viongozi wetu tena wakati mwingine hawana kosa lolote. Tunatengeneza chuki. Chuki hii itatugharimu sasa na hata baada ya uchaguzi. Tuwe makini sana kipindi hiki.
Taarifa kwa            Watanzania ambao wamekuwa na tabia ya kutukanana mitandaoni,            sheria mpya ya mitandao imeanza kufanya kazi jana Septemba            1.Hii ni sheria ambayo hakika tusipokuwa makini, wengi            tutajikuta katika mikono ya sheria.
        Mtu            anashiriki kusambaza kejeli kwa mtu ilimradi tu amkomoe            kutokana na chuki zake binafsi, si ustaarabu jamani.
Kutoijua sheria hakuzuii sheria kuchukua mkondo wake. Tujielimishe kupitia mitandao na sehemu nyingine ambapo sheria hii inapatikana.
        Kutoijua sheria hakuzuii sheria kuchukua mkondo wake. Tujielimishe kupitia mitandao na sehemu nyingine ambapo sheria hii inapatikana.
Niwatakie            maandalizi mema ya uchaguzi na Mungu aibariki Tanzania!
Ni mimi katika ujenzi wa taifa,
        Ni mimi katika ujenzi wa taifa,
............
Erick Evarist
        Erick Evarist
0 comments:
Post a Comment