September 21, 2015

  • UONGOZI MPYA WA KAMATI YA MISS TANZANIA YAANZA KUSAKA UPYA MAWAKALA WA MIKOA


    UONGOZI MPYA WA KAMATI YA MISS TANZANIA YAANZA KUSAKA UPYA MAWAKALA WA MIKOA
    Kutoka maktaba: Shindano la Miss Tanzania la kwanza mwaka 1967 ambapo mshindi aliibuka Theresa Shayo (No. 5) na ambalo lilikuwa la mwisho baada ya serikali kulipiga marufuku kwa kile kilichoitwa kukiuka maadili ya Mtanzania. Mwaka 2004 Miss Tanzania ikaibuka na mshindi alikuwa Ainda Maeda. Mwaka jana shindano hilo lilifungiwa kwa muda kabla ya Baraza la Sana la Taifa kuruhusu liendelee tena hivi karibuni.
    --------------------------------------------------------------
    Kamati ya Miss Tanzania inapenda kuwatangazia wadau wote wanaotaka kuandaa Mashindano ya urembo ya Miss Tanzania kwa mwaka 2016 kutuma maombi yao ya uwakala kuanzia sasa hadi tarehe 30 Novemba 2015 ndio mwisho wa kupokea maombi hayo. 
    Mashindano yatakayo fanyika ni ya mikoa tu, hakutakuwa na mashindano katika ngazi ya wilaya wala Kanda. 
     Sifa za kuwa Wakala wa Miss Tanzania ni pamoja na:

     1) Uwe na Kampuni iliyosajiliwa na Mamlaka husika ya Serikali. 
    2) Uwe na mtaji wa kutosha. 
     3) Uwe na uwezo wa kuandaa shindano katika ufanisi mkubwa. 
     4) Uwe mstari wa mbele katika kukuza sanaa za utamaduni nchini. 

     Wakala atakaye pitishwa na Kamati ya Miss Tanzania atapaswa kujisajili Baraza la Sanaa la Taifa.(BASATA) kabla hajapewa kibali cha kuandaa shindano. Wilaya za Mkoa wa D'salaam, Ilala, Kinodoni na Temeke zitapewa hadhi ya Kimkoa, ikiwa ni pamoja na Mkoa wa Elimu ya Juu. 
     Ada ya Uwakala ni shilingi milioni moja. 
     Ada ya Uwakala italipwa kwa Kamati ya Miss Tanzania baada ya maombi kukubaliwa na kupitishwa. Maombi yatumwe kwa barue pepe misstanzania2015@yahoo.com


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.