
Takwimu hizo zipo                  kwenye ripoti ya utafiti uliofanywa na Shirika la                  Kimataifa la Wahamiaji (IOM) uliofanywa kwenye Bandari                  ya Dar es Salaam na kuangalia namna jamii za watu wa                  maeneo ya bandari walivyo na uwezekano wa kupata                  maambukizi mapya ya ugonjwa huo kutokana na mwingiliano                  wa mataifa mbalimbali.
              Mshauri wa Mipango wa                  Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya                  Ukimwi (UNAIDS), Marie Engel katika uwasilishwaji wa                  ripoti hiyo uliofanyika leo jijini Dar es Salam alisema                  ingawa maambukizi yamepungua nchini, bado Dar ni                  miongoni mwa majiji yaliyoathirika zaidi.
              "Dar es Salaam ni jiji                  la sita kati ya 10 yaliyoathirika zaidi Afrika ikiwa na                  asilimia 6.2 za maambukizi mapya kwa mwaka. Maambukizi                  ya ndani yamepungua kwa kiasi na mpaka mwaka jana                  yalikuwa asilimia tano maeneo ya mjini na 7.2 vijijini                  huku wastani kwa nchi nzima ukiwa asilimia tano,"                  alisema Marie.
              Alifafanua kwamba vita                  dhidi ya ugonjwa huo vinaendelea na kwamba jamii ya                  kimataifa inaamini mpaka mwaka 2030 utakuwa historia                  ingawa kuna kazi kubwa inahitaji kufanywa ili kufikia                  lengo hilo la kuukabili Ukimwi ulianza kuenea miaka ya                  1980.
                
MWANANCHI.
            MWANANCHI.
0 comments:
Post a Comment