Akizungumza na wananchi wa                  Mkuranga wilayani Kisarawe, Duni Haji alisema Serikali                  ya CCM imeshindwa kuondoa tatizo la ajira na hivyo                  kusababisha vijana kujitumbukiza kwenye vitendo hivyo                  vya kihalifu, kama kuunda vikundi vya panya road.
                
                
              Alisema tangu Uchaguzi Mkuu wa                  mwaka 1995, CCM iliweka kwenye ilani yake nia ya kuondoa                  umaskini, lakini imeshindwa kutekeleza hadi leo na hivyo                  kusababisha vijana wengi kutopata ajira na kuingia                  kwenye uhalifu.
                
                
              "Walikuwa wapi kuondoa                  umaskini kwa miaka zaidi ya hamsini waliyotawala, leo                  wataondoaje," alisema Haji kwenye mkutano huo                  uliohudhuriwa na mamia ya watu kwenye Uwanja wa Godown,                  Mkuranga Mjini.
                
                
              Kuhusu kauli ya mgombea wa                  CCM, Dk John Magufuli ya kuwataka polisi kutoogopa                  majambazi na ikiwezekana kuwaua, Duni Haji alisema                  wangeanzia kwa majambazi walioko ofisini.
              "Kuna watu wanakaa ofisini                  ambao wamelifikisha Taifa hapa lilipo," alisema Duni                  Haji. Mfano wale majambazi waliochukua fedha za escrow,                  tena nasikia wengine wako Ikulu. Kama ni kuua majambazi,                  basi waanzie hao walio Ikulu."
                
                
              Alisema kutokana na kauli                  hiyo, Dk Magufuli anatakiwa kuogopwa na hafai kuwa Rais.
              "Hivi hajaingia Ikulu anasema                  maneno hayo, akiingia itakuwaje? Hao panya road                  watapona?" alihoji.
              Duni Haji, ambaye alihama CUF                  na kujiunga na Chadema katika mkakati maalum baina ya                  vyama hivyo viwili wa kujiandaa kushika dola,                  aliwashangaa wakazi wa Mkuramga kwa kuendelea kunywa                  maji ya kinyesi, akisema matatizo ya maji yanasababishwa                  na Serikali ya CCM
              Awali, mwenyekiti wa zamani wa                  CCM mkoani Dar es Salaam, John Guninita alimuelezea Dk                  Magufuli kuwa ni mtu asiyefaa kupewa urais, akimtuhumu                  kuhusika katika uuzwaji wa nyumba za Serikali na ujenzi                  wa barabara zilizo chini ya kiwango.
            
0 comments:
Post a Comment