June 15, 2014

  • UVCCM MKOA WA MOROGORO WAKINUKISHA LIVE LEO SOMA HAPA HABARI KAMILI LIVE!!


    UVCCM MKOA WA MOROGORO WAKINUKISHA LIVE LEO SOMA HAPA HABARI KAMILI LIVE!!

      Baadhi  ya wajumbe wa UVCCM  wakiwa na mabango yenye ujumbe wa kumpinga mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Moro Bi. Erieth Suta
     Wajumbe kutoka Wilya ya Gairo
     Kamanda wa UVCCM akisoma moja ya mabango hayo,
     Mjumbe kutoka Wilaya ya Kilombero
     Kutoka wilaya ya Ulanga
     Baadhi ya wajumbe hao wakiingia kwenye Kikao hicho cha baraza la Vijana mkoa kwa nyimbo na mabango ya kumpinga mwenyekiti wao
                                        Wakijiandikisha
     Mgeni rasmi wa Kikao hicho kamanda wa UVCCM Taifa Kingunge Ngombale Mwilu akiingia kwenye ukumbi huo wahotel ya Usambara iliyopo Nane Nane mkoani hapa
     Mzee Kingule akiwa na mwenyekti wa UVCCM Mkoa wa Moro Erieth Suta (kulia)
     Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Morogoroo Bi,Erieth Suta anayelalamikiwa na wajumbe akidaiwa kushindwa kuiongoza Jumuiya hiyo 
     Mwenyekiti huyo akimkaribisha mgeni rasmi
     Kamanda mkuu wa UVCCM Taifa mzee Ngombale Mwilu akizungumza kwenye Kikao hicho cha baraza la Vijana mkoa wa Moro
     Mzee Kingunge kisisitiza jambo kwenye hotuba yake jana 
     Baada ya kuzungumza Mzee Kingunge alisaini na kuwapa cheki ya shilingi milioni moja akichngia mfuko wa kusaidi Vijana wa Umoja huo,
    Pichani Kamanda huyo akiisaini Cheki hiyo
     Akimkabidhi mwenyekiti wa UVCCM mkoa

     Mwenyekiti huyo akiwaonyesja wajumbe wa mkutano huo
     Makamanda wa UVCCM Kutoka Wilaya zote za mkoa wa Morogoro wakisubiri kuapishwa
     Kamanda wa UVCCM Taifa Mzee Kingunge akiwaapisha makamanda hao
     Wakila kiapo cha kuutumikia Umoja huo

     Kamanda mkuu wa UVCCM Taifa mzee Kingunge akimvisha Skafu kamanda wa UVCCM Wilaya ya Morogoro Mjini Bw Paskal Kihanga ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Morogoro'MRFA'
     Kihanga akiwa na Mzee Kingunge baada ya kura kiapo
                                 
    Na Daustan Shekidele, Morogoro
    WAJUMBE wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi'UVCCM Mkoa wa Morogoro jana walimchana livekwa ujumbe wa mabango mwenyekiti wao wa mkoa Bi,Erieth Suta mbele ya kamanda mkuu wa taifa wa UVCCM Kingunge Ngombale Mwilu.

    Wajumbe wa Jumuiya hiyo kutoka wilaya zote za mkoa wa Morogoro walijipanga kwenye geti kuu la hotel ya Usambara ambapo kikao hicho cha Baraza la Vijana mkoa wa Morogoro kilifanyika ambapo mgeni wa kikao hicho kamanda wa taifa wa UVCCM Kingunge Ngombale Mwilu alisoma mabango hayo alipowasili kwenye hotel hiyo.

    Hata hivyo kwenye hotuba yake kamanda huyo wa taifa hakugusi ishu hiyo na kwamba baada ya kamandas huyo kufunga kikao hicho majira ya saa 11 jioni aliondoka  na wajumbe hao wareje kwenye kikao hicho huku ambacho watu wote wasiokuwa wajumbe hawakutakiwa kuingia kwenye kikao hicho.

    Kufuatia hali hiyo mwandishi wetu aliwashuhudi makachelo wa Polisi wakisambaa kwenye hotel hiyo kuimalisha ulinzi kwenye kikao hicho kilichomalizika saa nne usiku.

    Mjumbe mmoja wa kikao hicho alimweleza mwandishi wetu kwamba wajumbe hao wameshinda kumng'oa mwenyekiti huyo baada ya kukosa ushahidi wa tuhuma walizoeleke kwa mwenyekiti huyo.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.