June 23, 2014

  • TFDA waendelea kuteketeza bidhaa feki,wananchi wapata hofu.


    TFDA waendelea kuteketeza bidhaa feki,wananchi wapata hofu.
    Mamlaka ya Chakula na Dawa  kanda  ya kaskazini  imekamata  na  kuteketeza  shehena  ya  vyakula madawa  na  vinywaji  vyenye  madhara  kwa  wananchi  vilivyokuwa  vinaendelea  kutumika  katika maeneo  mbalimbali   ya  kanda  hiyo  na  imewaomba  wananchi  kutoa  ushirikiano  wa kukabiliana  na tatizo hilo.

     
    Mkurugenzi  wa  TFDA  kanda  ya kaskazini  Bw,Damasi Matiko   amesema pamoja  na  jitihada  zinazofanywa  na  mamlaka  hiyo  tatizo bado ni kubwa  na  ushirikiano  wa  wananchi unahitajika  ukiwemo  wa  kuwa  makini  katika  matumizi ya  bidhaa  zote  na  kutoa  taarifa  pindi  wanapobaini mapungufu.
     
    Afisa  afya  wa  manispaa  ya  jiji  la  Arusha  Bw Leny  Sumari  amesema  madhara ya matumizi  ya  bidhaa  bandia  ama  zilizopita muda  wake  ni makubwa  zaidi  kwa  watoto  na  ameikata  jamii  kuwa  makini  kwa  kuchunguza  zaidi   bidhaaa  zinauzwa  kwa  bei  rahisi.
     
    Kwa  upande  wao  baadhi ya  wananchi  akiwemo  Bw, Julius Moses  ,Peter  Ngusa , na  Simion Mollel pamoja na kuipongeza TFDA kwa  jitihada  wanazofanya  wamesema  bado ziko  taasisi  nyingine  za  serikali   ambazo  hazijatimiza  wajibu wake ipasavyo.
    chanzo ITV.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.