June 15, 2014

  • KIKUNDI CHA WAFUGAJI WA NG'OMBE WA KISASA WAAHIDIWA MKOPO NA COVENANT BENKI




    KIKUNDI CHA WAFUGAJI WA NG'OMBE WA KISASA WAAHIDIWA MKOPO NA COVENANT BENKI
     
     Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  Covenant  Bi.Sabetha Mwambenja  akitoa mfano wa  beiskali   wakati alipokuwa akiongea na kikundi cha wafugaji Ng'ombe  wa kisasa cha Kata ya Somangila Kigamboni jijini Dar es Salaam, kuhusiana na mradi huo.Benki hiyo inategemea kutoa  mkopo kwa kikundi hicho ili waweze kuendeleza ufugaji huo. Kulia ni Mratibu wa Wafugaji wa Ng'ombe  wa Kata ya hiyo  Getruda Mpelembe  na katikati ni  mtunza Hazina wa Kikundi hicho Jumanne Hussen na Kushoto ni Mwenyekiti  Taifa Wajasiriamali Dk.Dauda Salmin.
     Mratibu wa kikundi cha wafugaji wa Ng'ombe  wa kisasa Kata ya Somangila  Kigamboni jijini Dar es Salaam, Getruda Mpelembe (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  Covenant  Bi,Sabetha Mwambenja,Baada ya kuongea na kikundi hicho kuhusiana na maswala ya mradi wa ufugaji wa ng'ombe wa maziwa  wa kisasa  ambapo kikundi hicho kitanufaika na mkopo kutoka benki ya Covenant kwa ajili ya kuendeleza mradi huo wa ufugaji.   
     Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya wanawake ya Covenant  Bi,Sabetha Mwambenja  akisisitiza jambo  wakati alipokuwa akiongea na kikundi cha wafugaji wa Ng'ombe wa kisasa cha  Kata ya Somangila kiilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam, kuhusiana  na mradi wa ufugaji wa kisasa wa  ng'ombe wa maziwa   unaovihusisha vikundi vitatu  vya kata  hiyo ambapo wafugaji hao watapata mkopo wa kuendeleza mradi huo kutoka Covenant  benki.
     
     Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya wanawake ya Covenant Bi. Sabetha Mwambenja  akitoa mfano wa spoko za beiskali kwa kikundi cha wafugaji zaidi ya 45( hawapo pichani)wa Kata ya Somangila kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam, kuhusiana na mradi wa ufugaji wa Ng'ombe wa kisasa wa Maziwa.Benki hiyo inategemea kutoa mkopo kwa kikundi hicho ili kiweze kuendeleza ufugaji huo. Kulia ni  mtunza Hazina  wa Kikundi hicho Jumanne Hussen.



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.