July 18, 2014

  • Picha Kutoka IKULU:Rais Jakaya Kikwete Afungua Rasmi Jengo la Taasisi ya Kuzuia Rushwa-TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma


     Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti wa kumbukumbu wakati wa ufunguzi  rasmi wa ofisi za taasisi ya kuzuia rushwa TAKUKURU mkoa mjini Songea jana. Kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bibi Mary Mosha.
      Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na kaimu Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU Bibi Mary Mosha wakifunua kitambaa katika jiwe la msingi wakati wa ufunguzi wa jengo la ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma jana. Rais Kikwete yupo katika ziara ya kikazi  ya wiki moja mkoani Ruvuma
    Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi jengo la ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Ruvuma jana mjini Songea.Picha na Freddy Maro-IKULU



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.