Rose masaka-MAELEZO DAR ES SALAAM
          Mamlaka                ya  Udhibiti wa Usafirishaji  Majini na  Nchi Kavu                (SUMATRA) imetoa ufafanuzi kuwa  hajafikia muafaka  wa                kuwalazimisha abiria wa mikoani kutumia mchakato wa                 mbinu  mpya ya ukatishaji wa tiketi  za mabasi ya kwenda                mikoani kwa njia ya mtandao  ikiwemo wa simu za mkononi                kwa kuwa baadhi ya wamiliki wa mabasi wamegawanyika, na                bado haukidhi mahitaji ya sasa.
          Kauli hiyo imetolewa leo na Meneja wa                  Mawasiliano wa SUMATRA, David Mziray wakati akizungumza                  na mwandishi wa habari wa Idara ya Habari(MAELEZO) baada                  ya Chama Cha Kutetea  Abiria Tanzania(CHAKUA)                kuilalamikia, SUMATRA ndio inayochelewesha mchakato huo na                wameairisha kufanyika kikao cha wadau kilichotakiwa                kufanyika Mei30,mwaka huu.
          Malalamiko                hayo  yalitolewa na Mwenyekiti wa CHAKUA, Hassan                Mchanjama, alipokuwa akiongea na katika mkutano na                waandishi wa habari,uliofanyika leo kwenye ukumbi wa                Idara  ya Habari(MAELEZO).
          Aidha                kutokana na malalamiko hayo, Mziray alisema ni kweli kikao                hicho, kiliairishwa kutokana na sababu zisizoweza                kuzuilika huku akisisitiza kikao hicho kilikuwa cha                mashauriano na si cha kutoa uamuzi. 
          Mziray                aliongeza kwamba , hata hivyo  baadhi ya wamiliki wa                mabasi hayo, wamegawanyika kwani wapo wanaouunga mkono                utaratibu huo na  wengine wanaupinga kutokana kwamba                watakosa abiria , upatikanaji wa fedha unachukua muda                mrefu na mapato yao yatajulikana.
          "Hatuwezi                kuulazimisha utaratibu huo utumike kwa sasa kwa sababu                nilizotaja na pia  kuna baadhi ya  wananchi  hawatumii                simu za mkononi," alisema Mziray.
          Mziray                alisema waliishauri CHAKUA  watoe elimu kwa wamiliki hao                ili kuwezesha  utaraibu huo utumike kwa wale wanauunga                mkono na wanaoweza kuutumia, bali kwa abiria ambao ni                vigumu kutumia utaratibu wa zamani utumike.
           CHAKUA                iimetoa  malalamiko hayo kwa  mamlaka hiyo  baada ya                kuwasilisha mchakato huo kwa kumwandikia  barua , Waziri                wa Uchukuzi  Dkt. Harrison Mwakyembe , ambapo  uongozi wa                chama hicho  ulidai kuwa  aliiagiza SUMATRA  kuitisha                kikao  na wadau .
          Kikao                hicho   kiliitishwa Desemba 17,mwaka huu ,ambapo wadau hao                ambao ni Wamiliki wa Mabasi(TABOA), CHAKUA  na Jeshi la                Polisi la Usalama Barabarani walikubaliana kuanzishwa kwa                mchakato huo kwa  kukiitisha kikao na wadau baada ya miezi                mitatu.
          Aidha                Mchanjama amesema kuwa utaratibu waliougundua ni mzuri na                wenye manufaa kwa wamiliki , abiria na Serikali  kwani                itarahisisha muda wa kukata tiketi bila kwenda kituo cha                mabasi.
          Ameongeza                kwa kusema kuwa nauli zitakuwa ni halali na zilizoainishwa                na SUMATRA ili kuondoa kero kwa abiria ya kuongezewa nauli                hususani siku za sikukuu au shule zikifunguliwa au                kufungwa.
          "Utaratibu                huu unarisisha abiria kudai fidia pindi anapopata madhara                katika mabasi kama ajali ,kupotelewa na mzigo na magari                kugoma" alisema Mchanjama.
          Aliongeza                 kuwa kila kitu kitakuwa wazi katika mtandao, hivyo ni                rahisi kwa abiria kupata nyaraka za basi husika pindi                anapopata tatizo,pia mmiliki atafaidika kwa kupata mapato                moja kwa moja tofauti na sasa pesa zinapita mikononi mwa                watu wengi.
          Kuna                taasisi nyingi za serikali na watu binafsi ambazo zimekuwa                mfano mzuri katika utumiaji wa mtandao ambazo ni                TRA,TANESCO,DAWASCO na Benki mbalimbali.
        
0 comments:
Post a Comment