July 31, 2014

  • Pinda Mgeni Rasmi Mtwara Festival 2014


    Pinda Mgeni Rasmi Mtwara Festival 2014
     Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda  akiwa katika picha na Bw. Anic Kashasha, Mwenyekiti Mtendaji wa TACIN alipomtembelea  nyumbani kwake Oyserbay, Dar es Salaam, kumpa taarifa ya maendeleo ya maandalizi ya Mtwara Festival, itakayofanyika tarehe 16 - 17 Agosti, 2014 katika viwanja vya Chuo Cha Ualimu Mtwara(TTC). 
    Mh. Mizengo Pinda, anatarajiwa kuwa  Mgeni Rasmi wa Mtwara Festival, ambao ni mpango mkakati wa mawasiliano wa kuhamasisha wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi, kizitambua fursa shirikishi zinazosisimuliwa na uchumi wa gesi asilia. 
    Kauli mbiu ya Mtwara Festival ni "FURSA ZIMEFUNGUKA, TUZITAMBUE, TUJIANDAE, TUZICHANGAMKIE". Akizungumza mara baada ya kukutana na Waziri Mkuu, Bw. Kashasha alisema mpango huo wa elimu kwa umma, utachangia kwa kiasi kikubwa kutengeneza ajira na kipato kwa wananchi wa mikoa hiyo na hivyo kubadilisha hali za maisha ya wananchi hao.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.