December 19, 2015

  • Profesa Muhongo Kafuta Likizo Zote Za Wafanyakazi wa Tanesco.......Kawaagiza Pia Washushe Bei ya Umeme



    Profesa Muhongo Kafuta Likizo Zote Za Wafanyakazi wa Tanesco.......Kawaagiza Pia Washushe Bei ya Umeme

    Bei ya umeme inatarajia kushuka wakati wowote kuanzia sasa baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (pichani )kuliagiza Shirika la Umeme (Tanesco), kushusha gharama za nishati hiyo.

    Katika hatua nyingine, Waziri huyo amefuta likizo za wafanyakazi wa shirika hilo ili  washughulikie tatizo la umeme nchini huku akisisitiza kuwa hataki kusikia kukatika katika kwa umeme.

    Profesa Muhongo alitoa maagizo hayo  jana jijini Dar es Salaam wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika mtambo wa kuzalisha umeme wa Tegeta Gas Plant, ambapo alikwenda kwa ajili ya kukagua mitambo hiyo ili kuona kama yote inafanyakazi.

    Akitoa maelezo ya mtambo huo, Meneja Mohamed Kisiwa alisema wana mitambo mitano na wana uwezo wa kuzalisha Megawati 42 kila saa.

    Alisema gharama ya uzalishaji umeme kwa uniti moja ni Sh. 90 na wamekuwa wakiuza kwa Sh. 180 hadi 187.

    Profesa Muhungo alisema kwa maelezo ya meneja  huyo, inaonyesha umeme wanaozalisha wanapata faida mara mbili hivyo alisema kuna uwezekano mkubwa wa kushusha  gharama za umeme.

    Aliagiza maofisa wa wizara yake na wa shirika la Tanesco wakutane leo ili wajue umeme huo utashushwa kwa kiwango gani.

    "Utauzaje umeme mara mbili ya gharama za uzalishaji,  tunataka kuwapunguzia wananchi bei ya umeme  na kwenye mkutano wetu wa kesho (leo) tutajadili  kupunguza bei ya umeme..haya mahesabu hayajakaa sawa maana unazalisha uniti moja kwa Sh. 90 na kuuza kwa Sh. 180 tutajadiliana mpunguze," alisema.



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.