December 06, 2015

  • BALOZI SEFUE: MAAGIZO YA RAIS MAGUFULI HAYAVUNJI SHERIA YA UNUNUZI


    BALOZI SEFUE: MAAGIZO YA RAIS MAGUFULI HAYAVUNJI SHERIA YA UNUNUZI

    Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema maagizo ya Rais  Magufuli kutaka fedha zilizokuwa zitumike kwa matumizi yasiyo ya lazima, kupelekwa katika miradi mbalimbali ya maendeleo nchini, hayavunji sheria ya manunuzi wala utaratibu mwingine wa kisheria.
    Hivi karibuni,Rais Magufuli aliagiza sh.milioni 225 zilizokuwa nimechangwa kwa ajili ya hafla ya wabunge zipelekwe Hospitali ya Muhimbili kununua Vitanda na Mashuka.
    Aligiza pia Bilioni 4 zilizokuwa zitumike katika sherehe za Uhuru Disemba 9 zitumike kupanua barabara ya Mwenge- Morocco.

    Akitoa ufafanuzi wa barabara ya Mwenge-Morocco, Balozi Sefue  amesema mradi huo sio mpya na kwamba taratibu zote zilishafuatwa ikiwa ni pamoja na kuwalipa waliokuwa wamejenga  kando ya barabara.

    Amesema kilichokuwa kinakwamisha mradi huo ni  pesa.
    Akizungumzia sakata la wakuu wa mikoa na wilaya kuwanyima likizo wafanyakazi huku wengine  wakitiwa rumande kwa masaa  6, Balozi Sefue  amesema serikali haina taarifa rasmi hivyo akalitaka shirikisho la vyama vya wafanyakazi (Tucta) kuwasilisha malalamiko serikalini badala ya kuishia kulalamika katika vyombo vya habari.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.