December 26, 2015

  • HIVI NDIVYO POLISI WALIVYOYAKAMATA KIULAINI MAGUNIA HAYA YA BANGI



    HIVI NDIVYO POLISI WALIVYOYAKAMATA KIULAINI MAGUNIA HAYA YA BANGI
    Jeshi la Polisi mkoani Simiyu limefanikiwa kukamata magunia sita ya Bangi baada ya kutelekezwa na wamiliki walipoona askari polisi waliokuwa katika doria.


    Akiongea na waandishi wa habari jana katika kituo kidogo cha polisi cha Lamadi wilayani Busega kamanda wa polisi mkoani Simiyu Germini Mushy amesema.
     
    Amesema kuwa magunia hayo sita yenye uzito wa kilo 269 yalikamatwa kufuatia msako huo huku wamiliki wake watatu wakiyakimbia na kuacha baiskeli zao walipoona polisi.
     
    Aidha katika tukio lingine kamanda Mushy amesema kuwa mnamo disemba 22, mwaka huu majira ya saa 9 alasiri gari lenye namba T 366 VCJ kampuni ya J4 lilikutwa na begi likiwa na mirungi yenye uzito wa kilo 20 ndani yake.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.