October 01, 2014

  • DStv Bomba Yazinduliwa Tanzania



    DStv Bomba Yazinduliwa Tanzania
    MultiChoice Africa ina furaha kuwatangazia kuwa imezindua kifurushi kipya maalumu    kwa watanzania. Kifurushi hiki kimetengenezwa mahususi kwa watanzania kikiwa na      chaneli zaidi 65 za kitaifa na kimataifa zitakazotoa burudani  pekee kwa familia za  kitanzania.

    Kifurushi hiki kipya cha Bomba kina chaneli nyingi nzuri ikiwemo chaneli iliyozinduliwa   hivi karibuni ya Maisha Magic Swahili inayoonyesha filamu za kitanzania; chaneli ya  Telemundo inayojulikana kwa michezo ya kuigiza ya kimapenzi ya Amerika ya Kusini       pamoja na Nickelodeon na Disney Junior zinazoonyesha vipindi vya watoto.

    Meneja Mkuu wa MultiChoice Tanzania, Peter Fauel, alisema kuwa kifurushi kipya cha   Bomba kitagharimu kiasi cha TSh 17,000 tu kwa mwezi: " Uzinduzi wa kifurushi hiki cha Bomba ni jambo la furaha na msisimko sana kwetu, kuona kuwa sasa watanzania           wanaweza kupata kifurushi kinachokidhi mahitaji yao. 

    Kila wakati, MultiChoice inafanya jitahada za kubuni namna ya kuwapa wateja wetu uwanja mpana wa burudani. Sasa,     watanzania wameongezewa uwanja wa uchaguzi kwa bei iliyo chini na kiwango cha juu  cha burudani ikiwemo filamu, makala, habari, vipindi vya watoto, muziki, vipindi vya dini na michezo."

    Usikose ofa yetu ya uzinduzi huu - watakaojiunga watapata DStv ikiwemo gharama ya    ufundi kwa TSh 99,000 tu kwa kipindi maalum. DStv Bomba pia itakuwa na chaneli za     Africa Magic Epic Movies, Discovery World, CBS Action, CBS Reality na CBS Drama            pamoja  na Select Sport 1 na 2 kwa vipindi vizuri vya michezo.

    SuperSport Select na SuperSport Select 2 zitaonyesha ligi kuu ya Uingereza, Kombe la      klabu bingwa Ulaya, Ligi Kuu ya Hispania, Ligi kuu ya Ujerumani pamoja na riadha na      ngumi. SuperSport Blitz itawaletea habari zote za michezo.
    Kwa habari zaidi kuhusu burudani kwa ajili ya familia, tembelea tovuti:  


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.