October 29, 2014

  • BREAKING NEWS: KITU KINACHOSADIKIWA KUWA BOMU CHAKUTWA JIJINI DAR



    BREAKING NEWS: KITU KINACHOSADIKIWA KUWA BOMU CHAKUTWA JIJINI DAR
    Picha ya kitu kinachosadikika kuwa ni bomu kimegundulika maeneo ya Kijitonyama,  jijini Dar.

    Gari la uchafu likiwa linaenda kuchukua  uchafu eneo la tukio.

    Wananchi wakiwa eneo ambalo kitu kinachosadikiwa kuwa bomu kimeonekana.

    Askari polisi wakiwa eneo la tukio.

    Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Leonard Thomas amegundua kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu maeneo ya Kijitonyama, jijini Dar.



    Akizungumza na GPL Lenard alisema: "Nilikuwa naenda kuchoma moto taka ndipo nikaona kitu kama chuma kizito kama bomba ila kikanishangaza kiko kipekee nikiwa bado na shangaa mwenzagu akaja kuniambia kuwa ni bomu ndipo nikawajulisha polisi.



    Polisi walifika eneo la tukio na kuweka ulinzi wakati wakisubiri wataalamu wa mabomu wafike.
    (PICHA: GABRIEL NG'OSHA/GPL)


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.