Na Samwel Mtuwa.
Wakala wa Jiolojia                Tanzania , umefanikiwa kupunguza gharama za upimaji wa                sampuli za dhahabu katika maabara yake kwa kufanikiwa kwa                asilimia mia moja kuweza kutengeneza vikombe vya kupimia                dhahabu (Crucible) ndani ya maabara yake ya Jiolojia                mkoani Dodoma.
Kwa mujibu wa mtaalam wa                Jioloji katika Maabara ya GST, Bw. Philipo Momburi                alieleza kuwa hapo awali maabara ilikuwa inaagiza vikombe                vya kupimia dhahabu maabara kutoka nje ya nchi , jambo                ambalo lilikuwa likiingiza taasisi katika gharama kubwa ,                lakini baada ya utafiti wa kuandaa vikombe vya kupimia                sampuli ya dhahabu kukamilika umeweza kupunguza ghara kwa                asilimia hamsini (50%).
Bw. Momburi aliongeza                kuwa utafiti ulianza mwaka 1994 ambapo ulidumu kwa miaka                ishirini kabla ya kukamilika, ambapo baada ya kukamilika                 utekelezaji wake ulianza rasmi mwaka  2013, kutokana na                kukamilika kwa utafiti   GST imeweza kuongeza huduma za                kibiashara kwa kuongeza idadi ya upimaji wa sampuli kutoka                vikombe 20 mpaka 40 kwa siku.
Kwa upande wake                Mkurugenzi wa Maabara ya Jioloji GST Bi Augustine                Rutaihwa, aliongeza kuwa baada ya kuweza kutengeneza                vikombe hivyo , taasisi imeweza kupata  ubora mzuri wa                upimaji wa sampuli  katika maabara ya  GST , kuongeza                ujuzi kwa wataalamu , kutoa huduma kwa wakati , lakini pia                kuweza kutumia malighafi za ndani badala ya kuagiza kutoka                nje ya nchi.
Maabara ya upimaji wa                sampuli za  madini ilianzishwa mwaka 1929 kwa ajili ya                kuboresha shughuli za Idara hasa kwa upande wa uchambuzi                wa kimaabara wa sampuli za miamba , madini na maji.
Mtaalam wa Jiolojia Bw.                P.B Momburi akieonesha vikombe vya kupimia dhahabu katika                maabara ya Wakala wa Jiolojia Tanzania. 

0 comments:
Post a Comment