October 15, 2014

  • WAKALA WA JIOLOJIA TANZANIA , YAFANIKIWA KUKAMILISHA UTAFITI WA KUTENGENEZA VIKOMBE VYA KUPIMIA DHAHABU(CRUCIBLE)

    Na Samwel Mtuwa.

    Wakala wa Jiolojia Tanzania , umefanikiwa kupunguza gharama za upimaji wa sampuli za dhahabu katika maabara yake kwa kufanikiwa kwa asilimia mia moja kuweza kutengeneza vikombe vya kupimia dhahabu (Crucible) ndani ya maabara yake ya Jiolojia mkoani Dodoma.

    Kwa mujibu wa mtaalam wa Jioloji katika Maabara ya GST, Bw. Philipo Momburi alieleza kuwa hapo awali maabara ilikuwa inaagiza vikombe vya kupimia dhahabu maabara kutoka nje ya nchi , jambo ambalo lilikuwa likiingiza taasisi katika gharama kubwa , lakini baada ya utafiti wa kuandaa vikombe vya kupimia sampuli ya dhahabu kukamilika umeweza kupunguza ghara kwa asilimia hamsini (50%).

    Bw. Momburi aliongeza kuwa utafiti ulianza mwaka 1994 ambapo ulidumu kwa miaka ishirini kabla ya kukamilika, ambapo baada ya kukamilika  utekelezaji wake ulianza rasmi mwaka  2013, kutokana na kukamilika kwa utafiti   GST imeweza kuongeza huduma za kibiashara kwa kuongeza idadi ya upimaji wa sampuli kutoka vikombe 20 mpaka 40 kwa siku.

    Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maabara ya Jioloji GST Bi Augustine Rutaihwa, aliongeza kuwa baada ya kuweza kutengeneza vikombe hivyo , taasisi imeweza kupata  ubora mzuri wa upimaji wa sampuli  katika maabara ya  GST , kuongeza ujuzi kwa wataalamu , kutoa huduma kwa wakati , lakini pia kuweza kutumia malighafi za ndani badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi.

    Maabara ya upimaji wa sampuli za  madini ilianzishwa mwaka 1929 kwa ajili ya kuboresha shughuli za Idara hasa kwa upande wa uchambuzi wa kimaabara wa sampuli za miamba , madini na maji.
    Mtaalam wa Jiolojia Bw. P.B Momburi akieonesha vikombe vya kupimia dhahabu katika maabara ya Wakala wa Jiolojia Tanzania.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.