|                                                                  HIFADHI                    za taifa Tanzania (TANAPA) imetakiwa kuainisha maeneo                    yote yenye vivutio vya utalii ambayo yanawezekekana                    kuendelezwa na kuyatangaza kwa wananchi wote ili kila                    mwenye uwezo wa kuwekeza apewe nafasi.                                                   Hayo                    yalibainishwa na Waziri wa Maliasili na utalii, Lazaro                    Nyarandu, alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari                    katika mkutano wake uliofanyika ofisini kwa Mkuu wa                    Mkoa wa Mbeya katika mapumziko mafupi wakati akielekea                    mkoani Njombe kumuwakilisha Waziri Mkuu.                                                   Nyarandu                    alisema Serikali inamikakati ya kuhakikisha Watanzania                    ndiyo wanapewa vipaumbele vya kuwekeza katika sekta za                    utalii kwa kujenga nyumba za kulala watalii, kujenga                    makambi, kujenga na kuendeleza vivutio pamoja na                    kutembeza watalii.                                                   Alisema                    jambo hilo litasaidia kuinua sekta ya utalii nchini                    ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha watanzania kutembelea                    hifadi mbali mbali na sio kusubiri wageni kutoka nje                    ya nchi.                                                   Alisema                    ili kuongeza kasi ya watalii kuingia nchini kila                    mwananchi anapaswa kujifunza kukarimu wageni hususani                    wahudumu wa mahoteli ambao wamekuwa wakiwahudumia                    wageni kila wakati ili wawe na moyo wa kurudi tena.                                                   Kwa                    upande wa ujangili na mauaji ya Tembo Waziri Nyarandu                    alisema hivi sasa kuna mafanikio makubwa kutoka na                    kila Mwananchi kushiriki kulinda hifadhi na kuzuia                    majangili kuua wanyama ovyo kama ilivyokuwa awali.                                                   Alisema                    hivi sasa kuna ongezeko kubwa la Tembo tofauti na                    kipindi cha nyuma baada ya serikali yake kuweka                    mikakati kabambe ya kuwakabili wawindaji wote ikiwa ni                    pamoja na kuwafungia leseni wawindaji waliokuwa                    wakiwinda kinyume cha sheria na kuhusika kwenye mauaji                    ya Tembo.                                                   Aliongeza                    kuwa hata mfumo wa kukabiliana na ujenzi holela wa                    makazi na mahoteli ndani ya hifadhi za wanyama                    umechangia kuongezeka kwa uzalishaji wa Tembo ambapo                    alisema kwa takwimu za mwaka jana kuna ongezeko la                    tembo zaidi ya 70,000.                                                   Alisema                    hivi sasa Serikali haina idadi kamili ya tembo walipo                    nchini katika mbuga zote ambapo imeshaingia                    makubaliano na nchi wahisani ili kufanya sense ya                    Tembo na Faru ili Serikali iwe na idadi halisi ya                    wanyama hao nchini.                                                   Alisema                    kazi hiyo imeshaanza kufanyika ambapo Mwisho wa mwaka                    huu wanatarajia kupata majibu ambayo Serikali                    itawangazia wananchi wote ili wajue idadi ya Tembo na                    Faru waliopo katika kila hifadhi na mbuga za wanyama                    nchini.                                                   " Hivi                    sasa kusema ukweli kabisa mimi Waziri hata nikiulizwa                    swali leo kuwa tuna tembo wangapi nchini sina majibu                    kwa sababu hakuna mtu anayejua na wala hatujawahi                    kuhesabu jambo tunalitarajia kulifanya sasa" alisema                    Waziri.                                                   Mwisho.                                                     Na Mbeya yetu                  |             
0 comments:
Post a Comment