July 20, 2014

  • TAIFA STARS YATOKA SARE NA MSUMBIJI




    TAIFA STARS YATOKA SARE NA MSUMBIJI
     Mshambuliaji wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Samatta akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa Msumbiji katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
     Mbwana Samatta akiwatoka mabeki wa timu ya taifa ya Msumbiji. 
    Mshambuliaji nyota wa Taifa Stars, Mbwana Samatta akiwa katikati ya mabeki wa timu ya taifa ya Msumbiji. 


    Mshambuliaji wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Thomas Ulimwengu akimtoka beki wa Msumbiji, Zainadine Junior katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, wa kuwania tiketi ya Fainali za Afrika zitakazofanyika nchini Morocco mwakani. Timu hizo zilitoka sare ya 2-2. 
     Thomas Ulimwengu  akichuana na beki wa Msumbiji, Josemar Machaisse.

     Huniwezi...Mshambuliaji wa Taifa Stars, Thomas Ulimwengu akimtoka beki wa Msumbiji, Zainadine Junior.
     Mshambuliaji wa Stars, Khamis Mcha akiwa katika harakati za kufunga goli.
     Golikipa wa Stars, Deogratius Munishi akishangilia balo la pili la 
    Taifa Stars kwa kuonyesha fulana yake iliyokuwa ikisomeka 'Sisi ni Watoto wa Rais Kikwete'.



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.