July 18, 2014

  • MBUNGE JOSEPH MBILINYI "SUGU" AFANYA ZIARA MTAA WA TONYA - ITUHA, JIMBONI MBEYA MJINI


    MBUNGE JOSEPH MBILINYI "SUGU" AFANYA ZIARA MTAA WA TONYA - ITUHA, JIMBONI MBEYA MJINI
    •  APATA FURSA YA KUKAGUA SHUGHULI ZA MAENDELEO NA KUONGEA NA WAKAZI WA ENEO HILO
    • VIJANA WALIOCHUKUA KADI ZA CCM SIKU CHACHE ZILIZOPITA WAZISALIMISHA

     Vijana wa Mtaa wa Tonya - Ituha walimpokea Mbunge wao kuelekea Tonya

     Msafara wa Mbunge kuelekea Mtaa wa Tonya

    Mbunge alilakiwa na kikundi cha ngoma cha vijana
    Mbunge Joseph Mbilinyi akicheza ngoma baada ya kuwasili mtaa wa Tonya

     Msafara wa Mbunge ukaelekea kufungua Ofisi ya CHADEMA -Tonya

    Mh. Joseph Mbilinyi akiongea kabla ya ufunguzi rasmi wa Ofisi ya Tonya ambaye naye ameshiriki katika kuikamilisha

    Hapa Mbunge Sugu akijiandaa kuzindua ofisi

     Akisaini kitabu cha wageni kuonyesha kuwa ofisi imefunguliwa rasmi

     Baada ya zoezi hilo Mbunge alipelekwa na diwani kukagua eneo linalotarajiwa kujengwa daraja katika mtaa wa Tonya

     Hapo Mbunge Joseph Mbiliyi akiongea na wakazi wanaoishi kandokando ya daraja hilo

     Pia Mbunge alipata fursa ya kutembelea shule ya sekondari ambapo madarasa mapya yamejengwa

    Joseph Mbilinyi "Sugu" hapo akiwa katika mkutano wa hadhara katika Mtaa huo wa Tonya

     Wazee nao walikuwepo kusikiliza Mbunge akielezea shuhuli za kimaendeleo zilizofanyika jimboni

     Mmoja wa Kijana maarufu wa eneo hilo ambaye alichukua kadi ya CCM siku chache zilizopita alirudisha kadi  kwa Mbunge na kuelezea kuwa alichukua  kwa  kuwa alikuwa akihitaji shilingi 5,000 zilizokuwa zinagawiwa na CCM kwa vijana ili wagawiwe kadi hizo za CCM


     Wazee wakimshukuru Mbunge kwa kuwa mwakilishi wao mwema katika jimbo la Mbeya mjini

     Vijana wakikabidhiwa kadi za CHADEMA na mbunge wao


     Vijana wakiwemo ambao walirudisha kadi za CCM siku chache zilizopita wakiwa wanaonyesha kadi zao za CHADEMA walizokabidhiwa na Mbunge

     Wananchi wakionge na Mh. Joseph Mbilinyi mara baada ya mkutano wa hadhara

     Baadaye Mbunge Sugu alimalizia na kikao cha ndani na baadhi ya wakazi wa Tonya ambapo pia alipata fursa ya kupokea maoni na maswali na pia alitolea ufafanuzi mambo mbalimbali

    Kwahisani ya Joseph Mbilinyi blog




  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.