August 03, 2014

  • SBL YATANGAZA RASMI MSIMU WA ‘FIESTA 2014’



    SBL YATANGAZA RASMI MSIMU WA 'FIESTA 2014'
    1 (9)
    2 (8)Mkurugenzi wa  masoko wa kampuni ya   ya bia ya Serengeti   Ephraim Mafuru akigonga 'cheers' katika uzinduzi rasmi wa msimu wa Serengeti Feista 2014. Hafla hiyo ilifanyika Serena hoteli Dar es salaam. KAMPUNI  ya bia ya Serengeti  imetangaza kufungua rasmi msimu wa  Serengeti Fiesta kwa mwaka huu wa 2014. Akizungumza jijini Dare es salaam mwishoni mwa wiki katika hafla  ya chakula cha jioni Mkurugenzi wa  masoko wa kampuni hiyo  Ephraim Mafuru alisema msimu huo wa shangwe wameutangaza rasmi baada ya kumalizika kwa mwaka uliopita wa fedha na kuanza mwingine julai mosi  .
     Alisema kwa mwaka huu shangwe za Serengeti Fiesta zitaanzia mkoani Mwanza na kisha kufuatiwa na mikoa mingine hapa nchini.
     Aidha Mafuru alisema kuwa mbali na bia ya Serengeti ambayo ndiyo mdhamini mkuu wa Fiesta lakini pia wa watanzania wategemee kuburudika kwa bidhaa zingine mpya zinazotengenezwa na malighafi za hapa hapa nchini zitakazoingia sokoni siku chache zijazo.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.