August 26, 2014

  • TOCHI YA MBEYA YETU YAMULIKIA MITAA YA SAE , MWAMBENE NA ILOMBA JIJINI MBEYA


    TOCHI YA MBEYA YETU YAMULIKIA MITAA YA SAE , MWAMBENE NA ILOMBA JIJINI MBEYA
     Hii ni Barabara inayo anzia Sae kuelekea Mwambene, Wakazi wa eneo hili wanazingatia usafi 
     Hakuna Chembe ya takataka Mitaro kila kitu kipo sawa
     Usalama wa Barabarani umewekwa sawa kabisa kuna matuta ambayo hayawezi sababisha Gari likagonga chini hata kama likiwa fupi
     Haya ni Maeneo ya Mwambene 
     Hapa ni eneo mojawapo eneo la Mwambene ambapo Barabara hii ilikuwa ni korofi sana, sio kipindi cha masika wala cha ukame palikuwa hapapitiki lakini kwa sasa mambo safi kabisa inapitika vizuri.
     Ingawa Barabara imefika mpaka Mwambene kuna umuhimu wa hivi vibanda upande wa kushoto vikaondolewa na kuweka Maduka ambayo yatapendezesha mji.. Jiji hapo vipi?
     Hii ni Njia ya kuelekea Ilomba ukitokea Mwambene
     Moja ya Kona kali ambayo inatokea Ilomba kuelekea Mwambene 
     Haya maeneo ya Ilomba 
     Njia za wapita kwa miguu nazo zimeboreshwa
     Shughuli mbalimbali zikiwa zinaendelea 
     Hapa ni Makutano ya barabara inayoelekea Mwambene, Sae, Block Q na Ilomba 
    Bajaji zikiwa zimekaa katika mpangilio tayari kwa safari eneo la Mwambene


    Endelea kufuatilia Tochi yetu ya Mbeya yetu uone tutamulikia mitaa ipi

    PICHA NA MBEYA YETU


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.