Golikipa chipukizi wa                Timu ya Simba Sc,Manyika Peter 'Manyika Jr' (wa pili                kushoto) wakiwakabidhi Kombe Mashabiki wa timu hiyo mara                baada ya kuwasili kutokea visiwani Zanzibar kwenye                Mashindano ya Mapinduzi Cup,ambapo Simba waliibuka                mabingwa.
                Mashabiki wa timu Simba                SC wakishangilia ubingwa wao.Picha na Emmanuel                Massaka,Globu ya Jamii.
        Na Bakari  Issa ,Globu                ya Jamii Dar
        Klabu ya Soka ya Simba                leo hii imerejea jijini Dar es Salaam toka visiwani                Zanzibar ambapo imeibuka kinara wa Kombe la Mapinduzi jana                Januari13 katika mchezo uliopigwa usiku katika uwanja wa                Amaan.
        Akizungumza  mara baada                ya kuwasiri jijini Dar es Salaam,Mjumbe wa Kamati ya                Mashindano ya Klabu ya Simba,Juma Ngambili amesema  vijana                wamewapa  mashabiki wao kitu wanachokitaka licha ya kupata                ushindi kwa njia ya mikwaju ya penalty 4-3 na kusema kuwa                mashabiki wasubiri mambo mazuri toka kwao.
        "Tumeupokea ushindi kwa                mikono miwili,na tumewapa wapenzi wetu kitu wanachotaka na                tunawasihi mashabiki wasubiri mambo mazuri toka                kwetu,"alisema Ngambili
        Aidha,Ngambili amewatoa                hofu mashabiki wa Klabu ya Simba katika Ligi Kuu Soka                Tanzania Bara na kuwaambia kuwa watakuwa vizuri kwa                kuanzia na mchezo unaowakabili siku ya Jumamosi dhidi ya                Ndanda.
        Kwa upande wake nahodha                wa Simba,Nassor Masoud 'Chollo' amesema mchezo wao wa                fainali dhidi yao na Mtibwa Sugar ulikuwa mgumu na kusema                kuwa fainali ni fainali licha ya kuibuka na                ushindi.Naye,Golikipa chipukizi wa Klabu hiyo,Manyika                Peter 'Manyika Jr' amesema siri ya mafanikio yakwake na ya                Klabu ni kujituma zaidi na amewaomba mashabiki wa Simba                kuiunga mkono klabu yao.
        "Katika mchezo wa jana                nilitolewa kwenye dakika ya 90 naamini kama Kocha                angeniacha nidake mikwaju ya penalti ningedaka,tumenyakua                Kombe la Mapinduzi kutokana na wachezaji tulijituma na                nawasihi mashabiki wetu kutuunga mkono. 
        

0 comments:
Post a Comment