Kinara wa mtandao wa ujambazi katika            Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Njile Samuel (46) maarufu John,            amehukumiwa kifungo cha miaka 45 jela pamoja na kulipa faini            ya Sh. milioni tatu baada ya kukiri makosa yote mawili            yaliyokuwa yakimkabili.
         Mshtakiwa huyo alihukumiwa kosa la kwanza kifungo cha            miaka 15 jela na faini ya Sh. milioni tatu mbele ya Hakimu            Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Bariadi, Robert Oguda, baada ya            kusomewa mashitaka yake.
        Ilidaiwa katika shitaka la kwanza,            Januari 10, mwaka huu, saa 9:00 alasiri, eneo la Lyoma            wilayani Bariadi, Njile alikamatwa na risasi 272, bunduki aina            ya SMG na magazini saba.
        Katika shitaka la pili lililosomwa            mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Bariadi, Aidan            Mwilapa, mshtakiwa huyo alihukumiwa kifungo cha miaka 15 kwa            kupatikana na bunduki, huku kosa lingine alihukumiwa kifungo            kama hicho kwa kupatikana na umilikaji wa silaha bila kibali.
        Hata hivyo, adhabu hizo zitakwenda            kwa pamoja na mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka 30 jela.
        Wiki iliyopita, Makamanda wa Polisi            wa Mikoa ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga, walikutana jijini            Mwanza na kumuelezea Njile ni jambazi hatari ambaye katika            kazi yake alikuwa akiwaua wenzake baada ya kufanya uhalifu.
        
0 comments:
Post a Comment