MZIMU wa            sakata la akaunti ya Tegeta Escrow, limeendelea kuwatafuna            watuhumiwa  wa uchotwaji wa  mabilioni ya fedha za akaunti            hiyo baada ya watuhumiwa wengine watatu kupandishwa mchana huu            kizimbani katika mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.
                Waliopandishwa             ni Meneja  wa Misamaha ya Kodi  wa Mamlaka ya Mapato Tanzania             (TRA) Leonard Mutabingwa  ambaye anadaiwa kupokea rushwa ya            zaidi ya  shilingi bilioni moja kama zawadi kutoka kwa            Rugemalira, Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Mkombozi , Julius            Ruta, ambaye anadaiwa kupokea zaidi ya shilingi milioni 100             pamoja na  Ofisa Mwandamizi wa Tanesco, Steven Urasa,              anayetuhumiwa kupokea  zaidi ya shilingi milioni 100.
                bofya play video hapa chini
0 comments:
Post a Comment