Kushuka                  kwa bei. Ni mara ya kwanza tangu 2009 bei ya mafuta                  katika soko la dunia imeshuka kwa asilimia 50 tofauti na                  miaka ya nyuma.Meneja Mkuu PIC, Michaele Minja anasema                  iwapo itaendelea kuwa hivi hivi, huenda bei ikashuka                  zaidi.  Mamlaka ya                    Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imesema                    bei ya mafuta nchini inaweza kushuka kwa kiwango                    kikubwa ifikapo mwanzoni mwa mwezi Februari.Meneja uhusiano na                    mawasiliano wa mamlaka hiyo, Titus Kaguo alisema jana                    kuwa hilo linatokana na thamani ya shilingi kuporomoka                    dhidi ya Dola ya Marekani na pia muda ambao mafuta                    yanayouzwa sasa nchini, yalinunuliwa.Bei ya mafuta duniani kwa                    mara ya kwanza tangu mwaka 2009, imeshuka kwa zaidi ya                    asilimia 50.
              Dunia imeshuhudia tangu Juni                  mwaka jana, bei ya nishati hiyo ikishuka kutoka Dola 110                  ya Marekani mpaka Dola 60 kwa pipa moja la mafuta ghafi,                  hali inayoelezewa kuwa ingezisadia nchi zisizozalisha                  nishati hiyo.
          Lakini Kaguo alisema hilo                  halitaweza kuonekana kwa sasa hadi mwanzoni mwa                  Februari.
          "Bei imeshuka kwenye soko la                  dunia lakini thamani ya shilingi yetu inaendelea                  kuanguka kila siku, hii inasababisha kutoonekana kwa                  tofauti hapa nchini kwa kuwa bado tunaagiza bidhaa hiyo                  kwa Dola ya Marekani," alisema.
          Hata hivyo, Kaguo alisema                  kumekuwa na unafuu wa bei ya nishati hiyo katika miezi                  kadhaa iliyopita.
          "Bei inaweza ikawa nzuri zaidi                  kuanzia mwishoni mwa Februari kwa kuwa mafuta                  yanayoagizwa sasa ndiyo yatakuwa yameingia sokoni,                  lakini muhimu zaidi ni kuimarika kwa shilingi yetu dhidi                  ya Dola ya Marekani," alisema.
          Takwimu za Ewura zinaonyesha                  bei ya mafuta imekuwa ikipungua katika miezi miwili                  mfululizo.
          Mpaka Desemba 3, bei ya                  petroli ilikuwa imepungua kwa Sh149 kwa lita wakati                  dizeli ilipungua kwa Sh119 huku mafuta ya taa yakishuka                  kwa Sh106 kwa lita ikilinganishwa na Novemba.
          Meneja mkuu wa usimamizi wa                  uagizaji wa mafuta wa pamoja (PIC), Michael Mjinja                  alisema mwagizaji anayeleta mafuta kwa sasa alishinda                  zabuni hiyo mwezi Oktoba mwaka jana.
          "Kwa hiyo mafuta yaliingizwa                  tangu Novemba yakaanza kutumiwa Desemba," alisema.
            Alisema                    kampuni iliyoagiza mafuta yatakayotumika Februari,                    alishinda zabuni hiyo Desemba, 2014.
            "Mafuta                    yatakayoagizwa kwa ajili ya matumizi ya Februari,                    yananunuliwa kwa bei ya sasa kwenye soko la dunia                    lakini yatauzwa Februari," alisema.
            Alisema                    hata kama katika kipindi hicho mafuta yatapanda au                    kushuka, bei elekezi itakuwa ni ile ile iliyofungwa                    wakati wa utoaji wa zabuni.
            "Kama                    bei ya mafuta kwenye soko la dunia itaendelea kushuka                    ni matarajio yetu kwamba hapa nchini pia itaendelea                    kushuka," alisema.
            
0 comments:
Post a Comment