MUNGU ni mwema na ndiyo            maana leo wasomaji wa safu hii mnaisoma huku mkiwa na afya            njema. Tumhimidi Mungu aliyetuumba milele, amina.
Baada ya kusema hayo niseme machache kuhusu mikataba mibovu ambayo imeiingizia taifa hili hasara kubwa ambayo taifa linahujumiwa.
        Baada ya kusema hayo niseme machache kuhusu mikataba mibovu ambayo imeiingizia taifa hili hasara kubwa ambayo taifa linahujumiwa.
Mikataba hii inanifanya nijiulize,            baadhi ya watu, Watanzania wanasoma na kupewa nyadhifa za            kufanya kazi kwa niaba ya nchi walisoma ili kuiangamiza nchi            au kuitetea isizame?
Kati ya mwaka 1995 na 2007, nchi yetu ilighubikwa na mikataba ya uwekezaji ya kifedhuli, iliyosababisha mabilioni ya fedha kukwapuliwa na mafisadi wa ndani na nje ya nchi na kufichwa katika mabenki ya ughaibuni.
        Kati ya mwaka 1995 na 2007, nchi yetu ilighubikwa na mikataba ya uwekezaji ya kifedhuli, iliyosababisha mabilioni ya fedha kukwapuliwa na mafisadi wa ndani na nje ya nchi na kufichwa katika mabenki ya ughaibuni.
Baadhi ya mikataba hiyo hatari ya            uwekezaji, ni pamoja na ule wa mradi wa Independent Power            Tanzania Ltd (IPTL) na serikali, kupitia Shirika la Ugavi wa            Umeme nchini (Tanesco).
        Chini ya mkataba huo wa miaka 20,            nchi imeporwa mabilioni ya fedha na inaendelea kuchunwa na            kutupwa gizani kwa kukosa umeme, ingawa itaendelea kuilipa            IPTL zaidi ya shilingi bilioni 5.0 kwa mwezi kwa umeme            usiokuwepo, kuanzia mwaka 1999 hadi 2019.
        Walioiingiza nchi katika kashfa hiyo            wanafahamika kwa majina, lakini wamekumbatiwa na kutakaswa ili            watakasike na baadhi ya watu wasiokuwa na uchungu wa nchi hii            wanawaona ni wajanja!
Kashfa nyingine zenye kuhusisha mabilioni ya fedha, ni pamoja na ile ya EPA (ilihusisha shilingi bilioni 133), ununuzi wa rada na ndege mbovu ya rais kwa kile kilichoelezwa na Waziri wa Fedha wa wakati huo, Basil Mramba kwamba rais hawezi kupanda punda kama Yesu wa Nazareth. Ndege hiyo mbovu ilinunuliwa shilingi bilioni 40.
        Kashfa nyingine zenye kuhusisha mabilioni ya fedha, ni pamoja na ile ya EPA (ilihusisha shilingi bilioni 133), ununuzi wa rada na ndege mbovu ya rais kwa kile kilichoelezwa na Waziri wa Fedha wa wakati huo, Basil Mramba kwamba rais hawezi kupanda punda kama Yesu wa Nazareth. Ndege hiyo mbovu ilinunuliwa shilingi bilioni 40.
Nyingine ni ubinafsishaji wa Benki            ya NBC na uuzaji wa nyumba za serikali kwa bei ya kutupa,            pamoja na kuuzwa kwa Mgodi wa Makaa ya Mawe Kiwira, bila            kusahau sakata la mradi wa umeme wa kitapeli wa            Richmond/Dowans; Loliondo, ufujaji wa shilingi bilioni 150 za            Mfuko wa Uagizaji Bidhaa Nje (CIS) na mikataba mibovu ya            madini, kwa kutaja michache tu.
        Haya yametokea na hakika wasomi wote            waliohusika na hujuma hii wanapaswa kulaaniwa na wananchi wote            wazalendo wa nchi hii.
        Serikali imejitahidi kuficha ukweli            wa kashfa hizi lakini Mungu amewapenda zaidi wananchi na haya            mambo yakajulikana. Kashfa moja kabambe, inayohusu Mradi wa            Mgodi wa Meremeta ililipuliwa bungeni na  ilifikia Bunge            kuitaka serikali iwasilishe hesabu za kampuni hiyo kwa Mkaguzi            na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) ziweze kukaguliwa ili            kukata mzizi wa fitina.
        Tunaipa umuhimu wa pekee kashfa hii            ya Meremeta kwa sababu ni kielelezo cha wazi kwa serikali            kuhusishwa moja kwa moja katika uporaji wa rasilimali za taifa            na kugeuka mbogo kuwahadaa wananchi baada ya kugunduliwa kwa            kisingizio cha fedha zilizoporwa kutumikia usalama wa nchi.X
        Katika kashfa hiyo,  zaidi ya            shilingi bilioni 155 zililipwa kutoka Benki Kuu (BoT) kwenda            Benki ya NedBank ya Afrika Kusini kama malipo ya mkopo            uliodhaminiwa na serikali kwa mradi huo wa uchimbaji dhahabu.
Serikali ilibanwa na Bunge na kuagiza mahesabu yakaguliwe, haikutii na aliyekuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ( CAG) Ludovick Utouh, alinukuliwa baadaye akilalama: "Nitakagua nini wakati sijapata hesabu zenyewe kutoka serikalini…?
        Serikali ilibanwa na Bunge na kuagiza mahesabu yakaguliwe, haikutii na aliyekuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ( CAG) Ludovick Utouh, alinukuliwa baadaye akilalama: "Nitakagua nini wakati sijapata hesabu zenyewe kutoka serikalini…?
Kampuni ya Meremeta, ambayo baada ya            mambo kufichuka ilibadilishwa jina kiujanjaujanja na kuitwa            Tangold.
        Wabunge walikatazwa kuijadili kwa            sababu za kiusalama. Je, kuna ukweli gani kwamba Kampuni ya            Meremeta haizungumziki kwa sababu inagusa Usalama wa Taifa?            Je; ni kampuni ya serikali? Malipo hayo na mengine ndiyo            yaliyozua utata na Bunge kuagiza hesabu zikaguliwe.
        Napenda kutaja wazi hapa kwamba            Serikali ya Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kwa            namna yoyote ile, haihusiki na sakata zote hizi, ingawa            inazijua fika, hivyo,  imejitahidi kuziatamia bila mafanikio            kwa njia ya kufunika kombe mwanaharamu apite na mambo kama            hayo yamemgharimu aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji            Fredirick Werema.
        Serikali ifahamu kwamba kwa misingi            ya sheria, kitendo cha mtu kufunika kosa lililotendwa na mtu            mwingine, kwa lengo la kumwepusha sheria isichukue mkondo            wake, kinamfanya mtu huyo mwenye kutaka kumwokoa mwingine kuwa            mshiriki wa kosa hilo kwa kiwango sawa na cha mtuhumiwa halisi            wa kosa.
        Kwa hiyo, viongozi wanaowalinda au            kuwasafisha mafisadi wana hatia ya ufisadi uleule wa wale            wanaowaokoa.
        Nia ya kukumbushana ufisadi huu ni            kuwataka wanaokabidhiwa dhamana ya kulinda rasilimali za nchi            hii kuwa na uzalendo  wa kweli na kuachana na rushwa au hujuma            kwa taifa.
        Jipu limepasuka, siwezi                kuwa adui kwa kusema ukweli.
        
0 comments:
Post a Comment