January 06, 2015

  • AMUUA MWENZIE KWA SHOKA NA MWENYEWE KUJINYONGA BAADA YA KUDHURUMIWA SH MIL 87


    AMUUA MWENZIE KWA SHOKA NA MWENYEWE KUJINYONGA BAADA YA KUDHURUMIWA SH MIL 87
    Mkazi wa wilayani moshi mkoani kilimanjaro aliyekuwa akiishi songea kwa shughuli za kibiashara Bw. Emmanuel Moshi   amemuua mfanyabiashara mwenzake  aitwaye Didas Alfonce  kwa kumkata na shoka kichwani na kisha mwenyewe kujinyonga baada ya kudhulumiwa shilingi milioni 87.



    Kamanda wa polisi wa mkoa wa ruvuma ACP Mihayo Msikhela  amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema chanzo cha tukio hilo ni Wafanyabiashara hao kudhulumiana fedha za biashara za mbao walizopata.
     
    Kamanda mihayo amesema kuwa marehemu ameacha ujumbe  wa kurasa nne unaoeleza sababu ya yeye kuua na kisha kujiua.
     
    Katika ujumbe wake kamanda mihayo anasema marehemu moshi ametaja fedha alizokuwa akimdai mtu aliyemuua kiasi cha shilingi milioni  87  na Pia marehemu moshi  ameandika namba zake  za simu  kwa mawasiliano katika bahasha aliyowekea ujumbe huo.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.