Wanajumuia wa An Noor Leicester pamoja na                ndugu na marafiki kutoka ndani ya mji huo na mingine ya                Uingereza kama vile London, Leeds na Coventry Jumamosi                tarehe 4 Oktoba walijumuika kusherehea sikukuu ya Eid Ul                Adh-ha katika Masjid An Noor, Belgrave Gate.
        Ilikuwa ni sherehe ya kihistoria, ambayo                ilianza kwa Takbeer kisha Sala ya Eid, na kufuatiwa na                Khutba iliyotolewa na Imamu Mkuu Sheikh Saleh Juma.
        Kabla ya waumini kukumbatiana na                kupongezana, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Jumuia ya An Noor                Sheikh Mohammed Omar alisimama na kutoa taarifa ya                kihistoria, kwamba Jumuia imefanikiwa kwa uwezo wa Allah,                kutimiza lengo lake la kununua jengo inalolikodi, hapo                170a Belgrave Gate Leicester. ALLAHU AKBAR!
        Mwenyekiti akaarifu kuwa Jumuia imefanikiwa                kukusanya kiwango cha kutosha kulipa £175,000 kwa ajili ya                kukamilisha manunuzi. Pia imekusanya pesa zaidi kuweza                kununua kiwanja nyuma ya jengo kinachomilikiwa na                Halmashauri ya jiji la Leicester ili kupanua zaidi ukubwa                wa jengo. 
        Mwenyekiti akawashukuru wote wanaotoa                michango yao, na akaomba waumini wasiache kuendeleza                misaada yao kwani kazi inayofuata ni kubwa zaidi.
        Baada ya hapo ndipo Waumini wakapata nafasi                ya kupongezana, na hatimaye wote, wake kwa waume, wakaketi                kujipatia kifungua kinywa kwa pamoja.
        Kullu Am wa Antum Bikhayr!
        .jpg)
0 comments:
Post a Comment