July 11, 2014

  • PICHA ZIARA YA VIONGOZI WA TANZANIA SINGAPORE



    PICHA ZIARA YA VIONGOZI WA TANZANIA SINGAPORE
     Kutoka kushoto ni mkurugenzi wa taasisi ya biashara ya kimataifa iliyo chini ya wizara ya viwanda na biashara Singapore, Rahul Ghosh akibadilishana mawazo na Denis Rweyemamu na Linda Manu kutoka taasisi ya Uongozi ya Tanzania ambayo ndiyo iliyoandaa ziara ya mafunzo kwa makatibu wakuu na vionzoi waandamizi wa serikali ya Tanzania nchini Singapore.
     Baadhi ya makatibu wakuu walioko kwenye ziara ya mafunzo nchini Singapore yaliyoandaliwa na taasisi ya uongozi Tanzania, kutoka kushoto ni Dk Shabn Mwinjaka- Katibu mkuu wizara ya uchukuzi, Dk Ffolens Turuka- Katibu mkuu ofisi ya Waziri Mkuu,Dk Philip Mpango- Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Mipango na Dk Sivvacius Likwelile- Katibu Mkuu wizara ya Fedha.
    Ujumbe wa makatibu wakuu na viongozi waandamizi wa serikali ya Tanzania wakiwa katika mafunzo nchini Singapore, kuhusu uendeshaji wa shughuli za serikali kwa ushirikiano na sekta binafsi PPP mfumo ambao umeisaidia kimaendeleo nchi ya Singapore, Ziara hii inaratibiwa na taasisi ya Uongozi ya Tanzania- Uongozi Institute. (Picha zote na Vedasto Msungu Singapore)


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.