July 11, 2014

  • PICHA ZA VIONGOZI WALIOKO SINGAPORE KWA MAFUNZO



    PICHA ZA VIONGOZI WALIOKO SINGAPORE KWA MAFUNZO
     Picha ya pamoja ya viongozi waandamizi wa serikali ya Tanzania walioko nchini Singapore kwa mafunzo yaliyoandaliwa na taasisi ya Uongozi ya Tanzania. Picha hii imepigwa nje ya jengo la taasisi ya HYFLUX ya nchini Singapore, taasisi binaffsi inayojishughulisha na kusafisha maji ya baharini na maji machafu kwaajili ya matumizi ya majumbani. Singapore haina chanzo cha maji ya mito wala visima kwahiyo maji yake kwa matumizi ya majumbani huagizwa kutoka nchini Malayisia
     Nchi ya Singapore ni miongoni mwa nchi zenye majengo marefu duniani, nchi hii ni ndogo yenye ukubwa wa kilomita za mraba 716 tu eneo ambalo ni dogo hata kuliko ukubwa wa baadhi ya vijiji vya Tanzania hivyo inalazimika kujenga majengo yake kwenda juu yaani maghorofa kama yanavyoonekana na kuna majengo yenye ghorofa mpaka 72 kwenda juu.
    Baadhi ya viongozi waandamizi wa Tanzania walioko kwenye ziara ya mafunzo nchini Singapore wakipata maelezo ya namna mitambo ya kuchuja na kusafisha maji ya baharini kwaajili ya matumzi ya majumbani inavyofanya kazi,. Ziara ya viongozi hawa wa serikali ya Tanzania iliyoandaliwa na taasisi ya Uongozi inalenga kujifunza kuhusu uendeshaji wa serikali chini ya mfumo wa ubia kati ya serikali na sekta binafsi ambao umesaidia kuharakisha maendeleo ya nchi ya Singapore.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.