July 24, 2014

  • PPF na MSD wasaini makataba wa mpango wa "wekeza"



    PPF na MSD wasaini makataba wa mpango wa "wekeza"
     
     Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, (Kushoto), na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa, (MSD), Cosmas Mwaifwani, wakiweka saini mkataba wa "wekeza" kwenye hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya MSD, Keko jijini Dar es Salaam, Julai 23, 2014. Chini ya Mkataba huo, zaidi wa wafanyakazi 400 wa MSD wamejiunga na PPF. 
     Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, (Kushoto), akibadilishana hati na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa, (MSD), Cosmas Mwaifwani, baada ya kusaini mkataba wa mpango wa "Wekeza" kwenye hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya MSD jijini Dar es Salaam, Julai 23, 2014
     Mkurugenzi wa Operesheni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Asumpta Malya, (Kushoto), akikabidhi kadi mpya ya uanachama kwa mwanachama mpya ambaye ni mfanyakazi wa MSD, mara baada ya PPF na MSD kusaini makataba wa mpango wa 'Wekeza" kwenye hafla iliyofanyika makao makuu ya MSD, Keko jijini Dar es Salaam, Julai 23, 2014
     Mkurugenzi wa Operesheni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Asumpta Malya, (Kushoto), akikabidhi kadi mpya ya uanachama kwa mwanachama mpya ambaye ni mfanyakazi wa MSD
     Viongozi wa PPF na wenzao wa MSD, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutiliana saini mkataba ambapo MSD na PPF zimekubaliana kuanzisha mpango wa "Wekeza" ambapo wafanyakazi wa MSD sasa watakuwa wakichangia kwenye mfuko huo ili kujiwekea akiba na kujipatia mafao mbalimbali
    Viongozi wa PPF na wenzao wa MSD, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa MSD waliokabidhiwa kadi za uanachama wa Mfuko huo, mara baada ya kutiliana saini mkataba ambapo MSD na PPF zimekubaliana kuanzisha mpango wa "Wekeza" ambapo wafanyakazi wa MSD sasa watakuwa wakichangia kwenye mfuko huo ili kujiwekea akiba na kujipatia mafao mbalimbali


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.