March 03, 2016

  • TANESCO yadhamiria kufuta gharama za huduma kwa wateja (Service Charge).



    TANESCO yadhamiria kufuta gharama za huduma kwa wateja (Service Charge).
    Shirika la umeme nchini TANESCO limesema kwa sasa limejiimarisha  kimfumo na kiutendaji ili kuhakikisha wateja wake wote wanapata huduma bora za umeme na kwa wakati bila usumbufu wowote  huku mfumo katika vituo vyote vya kuuzia umeme ukiimarishwa.



    Wakati nchi kwa sasa ikiwa mguu sawa kuelekea kwenye kipato cha kati  yenye uchumi wa viwanda, nishati ya umeme wa uhakika ndiyo inayoweza kutimiza ndoto hiyo ya nchi, lakini TANESCO wanasema wamejipanga vema kimfumo tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
     
    Miongoni mwa mipango mikuu ya kurahisha huduma  ya utaoji wa nishati hiyo ya umeme,ni pendekezo la kufutwa kwa gharama za huduma kwa wateja, yaani  SERVICE CHARGE,huku tatizo la baadhi ya vituo vya kuuzia umeme  kushindwa kutoa huduma ipasavyo nalo likiwa tayari limekwisha kushughulikiwa.
     
    Afisa huyo mwandamizi wa TANESCO makao makuu  amewatoa hofu watanzania kuhusu nishati hiyo huku akisema ni lazima ya shirika hilo kuona  ndoto ya tanzania yenye viwanda  inatimia ikiwa na umeme wa uhakika.
     
    Wananchi wanasema  mipango ya uondoaji wa  gharama za huduma kwa wateja ni neema kwao kwani itawaondolea gharama nyingi walizokuwa wakitumia kununua umeme.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.