March 05, 2016

  • Mbowe Kuzungumza na Taifa Kupitia Waandishi wa Habari Makao Makuu CHADEMA Leo


    Mbowe Kuzungumza na Taifa Kupitia Waandishi wa Habari Makao Makuu CHADEMA Leo
    Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe leo atazungumza na Taifa kupitia mkutano wa waandishi wa Habari.

    Mkutano huo wa waandishi utafanyika saa 6 mchana makao makuu Kinondoni Ufipa.

    Kiongozi huyo mkuu wa upinzani nchini anatarajiwa kutoa tamko rasmi la maazimio ya Kamati kuu ya chama iliyokutana Machi 1

    Tayari vyombo vya ndani na nje ya nchi vimealikwa kwenye mkutano huo na imetakiwa ifikapo saa 5 asubuhi waandishi wote wawe wamekaa kwenye nafasi zao.

    Mwenyekiti huyo anabashiriwa mbali na mambo kadhaa lakini atatoa msimamo rasmi wa chama kuhusiana na hujuma ya watawala dhidi ya uchaguzi wa meya wa DSM

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.