Mzee                Yusuph (Kulia) akiongea na waandishi wa habari (hawapo                pichani) wakati wa utambulisho wa filamu yake ya Kwanza                iitwayo NITADUMU NAE ambapo filamu hiyo imeingia sokoni                leo Jumatatu na inasambazwa na Kampuni ya Proin Promotions                Limited, Kushoto ni Meneja Masoko wa Kampun ya Proin                Promotions Limited, Evans Stephen.
        Mzee Yusuph                akibadilishana Mkataba na Mwanasheria wa Kampuni ya Proin                Promotions Limited Halima Mara baada ya Kumaliza kutiliana                saini katika Mikataba.          Na Josephat Lukaza - Proin Promotions                Limited
        Hatimaye Mzee Yusuph                atambulisha rasmi ujio wake katika Tasnia ya Filamu leo                mara baada ya kuitambulisha filamu yake mpya na ya Kwanza                iitwayo NITADUMU NAE ambapo filamu hiyo ni moja ya filamu                ambazo zimetoka katika nyimbo zake.
          
              
        Akiongea na Waandishi wa                Habari Mzee Yusuph alisema "Filamu hii nimeitengeneza muda                mrefu sana na imetoka katika nyimbo zangu lakini                nilishindwa kuisambaza kutokana na kukosa Msambazaji                ambaye anaweza kukubaliana na vigezo vyangu lakini Kwa                bahati nzuri Proin Promotions imeweza kuwa na vigezo                ambavyo mimi nimekubaliana navyo na nimeridhika navyo ndio                maana nimeona wanaweza kusambaza filamu yangu" 
          
              
        Na Pia ameelezea sababu                kubwa ya yeye kuamua kufanya kazi na Proin Promotions ni                kwamba "Kampuni ya Proin Promotions hainunui hakimiliki za                wasanii ndio maana nimeona nifanye nao kazi"
        Vilevile Filamu ya Mzee                Yusuph ishaingia sokoni leo na inasambazwa na Kampuni                mahiri ya Proin Promotions Limited ambapo filamu hiyo                inapatikana Nchi nzima kuanzia leo.
          
              
        Mbali na hiyo pia Mzee                Yusuph amesema kuwa sasa anabadili nyimbo zake kwenda                kwenye filamu kwasababu nyimbo zake zote zina uwezo mkubwa                wakuwa filamu ndio maana kwa kuanza ameanza na Nyimbo yake                ya Nitadumu Nae.
         
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment