Na                    Baraka Mpenja, Dar                    es salaam
        TIMU ya Taifa ya                    Tanzania, Taifa stars  inatarajia kutua nchini kesho                    (julai 6) mwaka huu ikitokea nchini Botswana ili                    kuendelea na programu nyingine ya mazoezi.
         Stars                    inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iliweka                    kambi ya wiki mbili, mjini Gaborone kwa ajili ya                    kujiwinda na mechi dhidi ya Msumbaji kuwania                    kupangwa hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kucheza                    fainali za mataifa ya Afrika, AFCON mwakani nchini                    Morocco.
         Mechi                    hiyo muhimu kwa kocha wa Stars, Mholanzi, Mart Nooij                    itapigwa katika dimba la Taifa, julai 20 mwaka huu na                    wiki mbili baadaye mchezo wa marudiano utapigwa mjini                    Maputo nchini Msumbiji.
         Ikiwa                    ni sehemu ya kujipima ubavu, Stars ilicheza mechi ya                    kirafiki siku za karibuni na wenyeji wao Botswana na                    kuchapwa mabao 4-2.
         Mabao                    ya Taifa stars yalifungwa na Khamis Mcha `Vialli` na                    John Raphael Bocco `Adebayor`.
         Hata                    hivyo, matokeo hayo yalimfanya kocha Nooij ajue makosa                    ya kikosi chake na kuyafanyia kazi kabla ya                    kukabiliana na Black Mambas.
         Katika                    kambi ya Gaborone, Taifa stars ilimkosa winga wake                    machachari, Mrisho Khalfan Ngassa `Anko` aliyesafiri                    kwenda kufanya majaribio katika klabu ya Free State                    Stars inayoyoshiriki ligi ya Afrika kusini.
         Kocha                    Nooij alimuita Ngassa ili acheze mechi ya kirafiki na                    Botswana, lakini ilielezwa kuwa nyota huyo alikaidi na                    kwenda kufanya majaribio katika klabu hiyo inayonolewa                    na Mbelgiji Tom Saintfiet.
         Taarifa                    za uhakika zinasema kuwa Nooij amemuengua Ngassa                    kuelekea mchezo dhidi ya Msumbiji na tayari nyota huyo                    yupo nchini baada ya kumaliza majaribio yake Afrika                    kusini ambapo alifuzu, lakini uhamisho wake bado ni                    tatizo.
         Msumbiji                    wana historia ya kuiharibia Taifa stars katika mechi                    muhimu, hivyo ni muhimu kwa kocha kukisuka kikosi                    chake pamoja na watanzania kuisapoti timu yao.
         Stars                    ilifanikiwa kufuzu raundi ya pili ya hatua ya awali                    baada ya kuifunga Zimbabwe bao 1-0 katika dimba la                    Taifa jijini Dar es salaam na kulazimisha sare ya 2-2                    mjini Harare nchini Msumbuji.
         Msumbuji                    wao walishinda mabao 5-0 mjini Maputo na kutoka suluhu                    pacha ya bila kufungana dhidi ya Sudani Kusini                    ugenini.
         Mshindi                    wa jumla katika mechi hiyo atafuzu hatua ya makundi  ya                    kusaka tiketi ya kucheza AFCON mwakani nchini Morocco.
        
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment