July 11, 2014

  • JESHI LA POLISI NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WATAKIWA KUACHA KUKURUPUKA




    JESHI LA POLISI NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WATAKIWA KUACHA KUKURUPUKA
    imagesMahmoud Ahmad Arusha
    WAJUMBE wa Kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa wa Arusha(RCC) kimelitaka
    Jeshi la Polisi pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa kuacha kukurupuka na
    kutoa matamko ya haraka haraka  badala yake wachunguze kwa kina ili kubaini nini
    chanzo cha milipuko ya mabomu yanayoendelea kulipuka kila uchwao Jijini Arusha.Aidha wameshauri kuwepo kwa vikao vinavyoshirikisha wananchi mara kwamara ili kubaini matatizo mbalimbali yanayoweza kudhibitiwa ikiwemoufungaji wa kamera kwa wafanyabiashara wenye biashara zaidi yaSh,milioni 50 hadi 100 na kuwataka kufuatilia kwa ukaribu sehemu mbalimbali zenye mikusanyiko kama zinatumia vifaa vya ukaguzi.

    Hayo yalisemwa jana Jijini hapa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless
    Lema , Mbunge wa Arumeru Magh
    aribi ,Goodluck Ole Medeye pamoja na
    Askofu wa KKKT Dayosisi ya Meru, Dk, Paulo Akyoo wakati wakichangia kwenye kikao hicho.
    Lema alisema matukio yanayotokea ya mlipuko wa mabomu Jijini hapa si
    matukio ya masuala ya siasa bali ni matukio yanayodhuru jamii ambayo
    ni muhimu kwa maisha ya kila siku hivyo ni vyema polisi wanapopewa
    taaarifa waifanyie kazi badala ya kuchukulia kuwa taarifa hizo ni za
    kawaida huku milipuko ikiendelea kutokea .
    Alisema ni vyema sasa kila mfanyabiashara kununua kamera za CCTV ili
    kuweza kubaini matukio mbalimbali ya kihalifu pamoja na ulipuaji wa
    mabomu ambao kwa hivi sasa ni tishio kwa Jiji la Arusha pamoja na
    jamii kwa ujumla.
    "Usalama wa wananchi uko wapi kila mara mabomu mabomu na baadhi ya
    wanasiasa wanatumia masuala haya ya mabomu kama ni umaarufu wa kisiasa
    hapana tuache mambo haya tunataka matukio haya yachunguzwe kwa kina
    ili kujua kiini cha tatizo hili ni nini na si kudai masuala ya kisiasa
    au la''
    Naye Askofu, Dk Akyoo alisema ni vyema sasa ile desturi ya ulinzi na
    usalama ngazi ya kata ikarejeshwa na vikao vya mara kwa mara ili
    kudhibiti matukio ya uhalifu yanayotokea mara kwa mara Jijini hapa na
    kutoa rai kwa polisi kuhakikisha wanajenga urafiki na wananchi badala
    ya uadui ili hata taarifa zinapotolewa wazifanyie kazi na kutoa majibu
    sahihi kwa wananchi.
    Naye Medeye alisema kuwa Arusha inastahili kuangalia kwa jicho la pekee
    kuhusu masuala ya milipuko kwani mabomu yakitokea mji unakuwa si
    shwari hivyo ni vyema Kamati ya Ulinzi na Usalama wakachunguza masuala
    haya kwa makini na kutoa majibu sahihi ikiwemo kumshauri Rais Jakaya
    Kikwete juu ya nini kifanyike ili kudhibiti matukio haya kama vile
    tukio la ulipuaji wa bomu lililotokea ubalozi wa Marekani miaka kadhaa
    iliyopita.
    Hata hivyo  Mwakilishi wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Edith
    Salvas aliomba ushirikiano kwa wananchi ili kubaini wale wote
    waliohusika na matukio ya ulipuaji wa mabomu Jijini Arusha ilikuweza kudhibiti matukio hayo yalichukuwa kasi hivi sasa.
    Naye Mkuu wa Wilaya ya Arusha, John Mongela aliyekuwa akiongoza kikao
    hicho aliongeza kuwa inabidi vyombo vya ulinzi na usalama vikafanyia
    kazi michango hiyo ili kuja na majibu yatakayoweza kutoa picha kwa
    wananchi ,kikao  hicho kilihudhuriwa na wabunge mbalimbali wa mkoa wa
    Arusha, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Saning'o Ole Telele pamoja na
    wadau mbalimbali wa Jiji la Arusha.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.