December 18, 2014

  • MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA AKUTANA NA RC ARUSHA


    MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA AKUTANA NA RC ARUSHA DSC_0175
    Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliyeteuliwa hivi karibuni, Daud Felix Ntibenda alipomtembelea ofisini kwake kuzungumzia miradi mbalimbali inayofadhiliwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa mkoani humo.
    DSC_0170
    Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (kushoto) akisaini kitabu cha wageni wakati Mkuu wa Mkoa na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wkibadilishana mawazo kabla ya kuanza mazungumzo yao.
    DSC_0178
    Mkuu wa Mkoa wa Arusha aliyeteuliwa hivi karibuni, Daud Felix Ntibenda akizungumza na Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) aliyeambatana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu.
    DSC_0185
    Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo na uongozi wa mkoa wa Arusha ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Daud Felix Ntibenda (kulia) na kushoto ni Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha, Addo Mapunda.
    DSC_0189
    Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (kushoto) katika picha ya pamoja na uongozi wa mkoa wa Arusha.
    DSC_0198
    Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha, Addo Mapunda akifafanua jambo kwa Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Daud Felix Ntibenda.


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.