July 12, 2014

  • Ahadi za JK 2010 - 2015 - Tufanye Tathmini Ndogo zipi zimetekelezeka?

    Ni Takribani mwaka mmoja tu sasa umebaki ili kutimia ile miaka mitano ya utawala wa JK. Na nilipojaribu kuingia kwenye kumbu kumbu zangu, nikaamua kuibuka na vitu vilivyowafanya watanzania wakaamua kumchagua JK kuongoza tena. TUjadili, ni ahadi ipi kati za hizi imetimia, na kwa ubora gani? Maana kutimia tu si hoja, hoja ni ufanisi, na ubora wake kwa waahidiwa!

    AHADI - ALIITOA AKIWA WAPI...

    1.      Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora

    2.      Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini

    3.      Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga

    4.      Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga

    5.      Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma

    6.      Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini

    7.      Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma

    8.      Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera

    9.      Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera

    10.  Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini

    11.  Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini

    12.  Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera

    13.  Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera

    14.  Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera

    15.  Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya

    16.  Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera

    17.  Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali

    18.  Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza

    19.  Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza

    20.  Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita

    21.  Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba

    22.  Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro

    23.  Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini

    24.  Kujenga bandari Kasanga – Rukwa

    25.  Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea

    26.  Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya

    27.  Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga

    28.  Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa

    29.  Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro

    30.  Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini

    31.  Kuboresha barabara za Igunga - Tabora

    32.  Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu

    33.  Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini

    34.  Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara

    35.  Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa - Musoma

    36.  Kulinda haki za walemavu - Makete

    37.  Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini

    38.  Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha

    39.  Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini

    40.  Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora

    41.  Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini

    42.  Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma

    43.  Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido

    44.  Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga

    45.  Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini

    46.  Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma

    47.  Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido

    48.  Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro

    49.  Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara

    50.  Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini

    51.  Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini

    52.  Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa

    53.  Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa

    54.  Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa

    55.  Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi -Ifunda

    56.  Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara

    57.  Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa

    58.  Ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii - Kibandamaiti Mjini Zanzibar

    59.  Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar

    60.  Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti

    61.  Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma

    62.  Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma

    63.  kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma

    64.  Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma

    65.  Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam

    66.  Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara

    67.  Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha

    68.  Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa - Kibaha

    69.  Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda - Kibaha

  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.