December 09, 2016

  • Aubemeyang na kila dalili za kwenda Real Madrid.

    aube

    Real Madrid ina uwezo wa kusajili karibia wachezaji wote kwa gharama yoyote ambayo ni reasonable kwa wachezaji nyota duniani kwa sasa hivi.

    Habari za Aubameyang kujiunga na Real Madrid zimeongelewa sana na kwa kiasi kikubwa mchezaji mwenyewe anaendelea kuzibariki siku hadi siku. Baada ya mechi ya UEFA, Aubemeyang aliulizwa maswali na mwandishi wa habari na majibu yake yaliendelea kuonyesha kwamba yeye ni mchezaji wa Real Madrid kwa muda kadhaa ujao.

    Mwandishi alimuuliza kama atakuja kucheza Real Madrid, Aubameyang alimjibu kwamba alimpa ahadi babu yake kwamba siku moja atakuja kucheza hapo. Babu yake alikua anaishia nje kidogo ya makao makuu ya club ya Real Madrid. Hivyo basi amekua shabiki wa club hiyo kwa muda mrefu.

    Swali lingini mwandishi alimuuliza kwamba "Nimwambie Florentino Perez kwamba unataka kuwa ndani ya Real Madrid?". Mwandishi huyo alisema kamba Aubameyang alijibu ndiyo.

    Pia kupitia instagram account yake Aubameyang aliandika ujumbe wenye utata kidogo na picha ya mechi dhidi ya Real Madrid. Pierre aliandika "Nafikria kitu kimoja tu. Natumaini umeliona lile goli Babu".

    Wachambuzi wa mambo wanasema kumuona Aubameyang ndani ya kikosi cha Real Madrid halitakua jambo la kushangaza ndani ya muda mfupi ujao.



  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.