November 12, 2014

  • MTOTO WA RAIS KIKWETE AKANUSHA KUMILIKI KAMUNI YA SIMBA TRUST



    MTOTO WA RAIS KIKWETE AKANUSHA KUMILIKI KAMUNI YA SIMBA TRUST
    Mtoto wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Miraji Kikwete usiku wa Nov 11 2014 ameeleza kuhusu ishu inayosambazwa kwamba anamiliki kampuni ya Simba Trust iliyopo Australia akishirikiana na dada yake.Kufuatia tuhuma hizo Miraji alipost maandishi akikanusha hiyo ishu akisisitiza kwa eleweke hivi ningekuwa napokea milioni 100 kwa siku wallahi ningeshukuru kwa mola ila siwezi kuchukua fedha kinyume na haki ninayo stahili'
    'Katika jambo lililonishangaza ni hizi tuhuma za kuwa ninamiliki kampuni ya Simba trust ya Australia mimi na dada yangu Salama, naona sasas mmeishiwa hoja na kuanza kuzusha mambo, sijawahi kufika Australia na sina kampuni ninayomiliki na dada yangu, lakushangaza kwanini PAP wanilipe pesa bila sababu maalum'
    'Sina pesa nyingi kiasi hicho, kidogo ninachokipata ni kwa jasho langu, sijawahi na sitodiriki kupokea pesa ambazo si haki yangu kupata, acheni kupandikiza chuki zisizo na ukweli wowote, atakaethibitisha basi na aonyeshe hilo kwa vielelezo na ushahidi, chuki hazijengi, kweli umeishiwa hoja na mambo ya msingi ya kujadili'

    .


  • 0 comments:

    Post a Comment

    Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.