Tunakujali, Tunakuthamini na Pia Tunakupenda!

Showing posts with label Utabibu na Afya. Show all posts
Showing posts with label Utabibu na Afya. Show all posts

July 16, 2014

  • FAHAMU DAWA YA KUTUNISHA MISULI INAYONG'ANG'ANIWA NA VIJANA WA KITANZANIA



    FAHAMU DAWA YA KUTUNISHA MISULI INAYONG'ANG'ANIWA NA VIJANA WA KITANZANIA

    Pengine  ni katika harakati za kuutafuta utanashati  au  ukosefu wa ajira,  na huenda ikawa ni mtindo wa kimaisha kwa vijana wengi hapa nchini na duniani kote wanaotunisha misuli. Hata hivyo wanaume walio katika harakati za kutunisha misuli au kupata maumbo yenye miraba minne, wamekuwa wakitumia dawa ili kuyapata maumbo hayo badala ya kufanya mazoezi  ya viungo.

    Vijana wengi hivi sasa  wananunua kwa wingi dawa za kutunisha misuli maarufu kama 'doping' kwa sababu zinazotajwa kuwa ni kutafuta ajira kama vile ulinzi kwenye kumbi za starehe, ulinzi wa watu maarufu(bodyguard) na wengine mashindano ya kunyanyua vitu vizito huku wengine wakiutafuta utanashati.
    Steroids
    Wataalamu wa afya wanataja baadhi ya dawa zinazonunuliwa na wajenga misuli kuwa niAnabolic Steroids, ambazo husaidia kujaza misuli na kutochoka haraka.
    Ripoti  ya Wizara ya Afya na Huduma za Jamii ya Marekani inaeleza hivi: 
     Dawa za steroids za kuongeza ukubwa wa misuli ni kemikali zinazohusiana na homoni za kiume (tetosterones). Dawa hizo huchochea ukuzi wa misuli na kustawi kwa maumbile ya kiume. Wavulana wanapobalehe homoni hizo huongezeka na kubadilika na hivyo kuchochea mabadiliko ambayo humfanya mvulana awe mwanamume. Nyingine ni Creatine ambazo huuzwa katika hali ya unga unga na kama ilivyo Steroids, dawa hii nayo hujenga misuli na kuondoa maumivu ya mwili na Human Growth Hormone, vichocheo ambavyo hukuza misuli ya mtu kwa wiki chache tu.
     Dawa nyingine zenye nguvu na zinazotumiwa zaidi na wanaume wanaotaka kujenga misuli ni Optimal Stack, Precision Power, Estoforce Edge, Muscle Ex Edge na Muscle Rip Edge.
    Miaka ya 70, watunisha misuli wengi akiwemo Arnold Schwazenerger, walikiri kutumia Steroids kama dawa zinazowasaidia kukuza misuli yao   hata hivyo mwaka 1990,  Marekani, ilianzisha sheria ya kuzuia dawa za Steroids na kuiweka katika kundi la dawa zilizopigwa marufuku.
    Uchunguzi Fichuo tz umebaini kuwa baadhi ya vijana hutumia dawa za vichocheo vya wanaume  kama testosterone kukuza misuli hiyo. Wengi hutumia dawa hizo kwa kiwango kikubwa kiasi cha mara 10 hadi 100 zaidi ya kile ambacho daktari anaweza kukuandikia.
    Wengi huzipata dawa hizi nchini Afrika Kusini ambako huletwa na watu binafsi na kuzisambaza katika nyumba za mazoezi (gym) ambako vijana wengi hufanya mazoezi ya kujenga vifua.
    Gosbert Msuya, mlinda mlango wa klabu ya muziki ya Maisha, anakataa kutumia dawa za kutunisha misuli, lakini anakubali kuwa wapo vijana wanaotumia dawa hizo kwa sababu mbalimbali kubwa ikiwa ni ajira na mwonekano. 
     Sasa ukiwa na mwili mkubwa unapata kazi za kuwalinda watu maarufu, kulinda 'stage' pindi wanamuziki wanapoburudisha. Ajira nyingine ni wakati wa maadhimisho makubwa ya kitaifa, kucheza filamu, na mwonekano mzuri
    anasema Msuya.
    Kijana anayekunywa dawa hizi huweza kuongezeka kilo tano hadi 15 ndani ya miezi miwili. Mzunguko na msukumo  wa damu yake huongezeka kiasi cha asilimia 20, jambo linalosababisha misuli yake kujaa.
    Misuli hii huonekana wazi zaidi kwani dawa hizi husaidia kuchoma kalori kwa kiasi kikubwa  n husababisha mwili  kupoteza mafuta mengi.


  • DAWA ZA DICLOPA NA DICLOFENAC ZADAIWA KUWA NI HATARI KWA MATUMIZI YA BINADAMU




    DAWA ZA DICLOPA NA DICLOFENAC ZADAIWA KUWA NI HATARI KWA MATUMIZI YA BINADAMU

    Dawa za Diclopa na Diclofenac zadaiwa kuwa ni hatari kwa matumizi ya binadamu!
    Radio Dutch Velle ya mjini Kolon Ujerumani jana ilitangaza kuwa Dawa Diclopa na Diclofenac ni hatari kwa matumizi ya binadamu, Imegundulika Vidonge hivyo husababisha kansa ya Ini na Ubongo,Ugonjwa wa moyo,
    Kiharusi, Vidonda vya Tumbo au kifo cha ghafla.



    Chanzo: Radio Dutch Velle


  • July 06, 2014

  • Njia Tano za kulala Vizuri Usingizi

    You may think your sleep routine is as simple as PJs on, lights out, but really, most of us are not sleeping correctly. And what’s worse, letting proper sleep habits fall by the wayside is one of the easiest ways to put your health at risk. It’s time for a re-education: Follow these five simple rules for better, healthier rest. 

    Rule #1: Set a 7-days-a-week schedule. “Regularity is vital—go to bed at the same time every night and wake up at the same time naturally, including weekends,” says Equinox advisory board member and sleep expert James B. Maas, Ph.D., author of Sleep for Success!. “You have one biological clock, not one for the work week and one for the weekend. You must synchronize the circadian sleepy phase of your biological clock with your bedtime, and the alert phase with your waking life, otherwise a yo-yo schedule will give you symptoms similar to those of jet lag—daytime drowsiness, slow reaction time, impaired cognition, moodiness, lack of energy.” To know your personal sleep time, Maas suggests choosing a time that’s a minimum of eight hours before you need to wake up, and following it for one week straight. Still tired? That means you need an earlier bedtime (try just 15 to 30 minutes more). Once you can get up in the morning alarm-free and feel alert most of the day, you’ve hit it just right.

    Rule #2: Cut caffeine after 2 p.m. Late afternoon is when the body has a temporary drop in focus and why the urge to have some caffeine often strikes. While a buzz will definitely perk you up, it could linger long after you’ve left work. “Six hours after your last sip of caffeine, it’s still in your body so it’s crucial to keep your daily intake at under 300 mg—like three small cups—and to avoid it anytime after 2 p.m.,” says Maas.

    Rule #3: Control your body temperature. Overheating is a major sleep disruptor, according to Maas. Research shows that 65 degrees is the sweet spot temperature for a good night’s rest, which means you need to do you what you need to in order to keep it in check—set your thermostat, choose a lighter blanket and PJs, or use a fan. 

    Rule #4: Dim, if not ditch, your devices. As addictive as bedtime Twitter scrolling may be, it’s the emitted light that’s the problem. “Blue light hits the spectrum of day light—it’s an alerting mechanism—so it’s like going in the sun,” says Maas. Translated: It wakes you up. “Avoid any electronics at least one hour before bed so that you don’t block melatonin, the sleep hormone that’s secreted when you’re in the dark, and delay the onset of sleep,” says Maas. If you can’t cut the habit completely, at least dim the light on your devices until you can ease yourself off one hundred percent.

    Rule #5: Just say no to drugs. “Prescription sleep medications can actually be really dangerous—they can cause heart attacks, strokes and even death,” says Maas. “I always try to get patients off of pills.” Maas says that if you think taking melatonin helps you sleep, then it probably does and regardless, it won’t cause any harm. But for some, it simply isn’t effective and the current research is unreliable—some people who are given a placebo will sleep as long as those given the real thing.

    Photography by Matt Jones / Trunk Archive

  • June 18, 2014

  • MAAMBUKIZI YA VVU KITAIFA KWA WANAWAKE NI ASILIMIA 6.2 NA WANAUME NI ASILIMIA 3.8.



    MAAMBUKIZI YA VVU KITAIFA KWA WANAWAKE NI ASILIMIA 6.2 NA WANAUME NI ASILIMIA 3.8.
    Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam Bi. Terezia Mmbando (kulia) akitoa taarifa ya hali ya maambukizi ya VVU na Ukimwi katika jiji la Dar es salaam kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho alipotembelea maeneo mbalimbali ya jiji hilo kuangalia hatua zilizofikiwa katika kupambana na ugonjwa huo katika ziara yake ya siku nne.
    Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Bw. Raymond Mushi akitoa tathmini ya hali ya maambukizi ya VVU katika jiji la Dar es salaam na hatua zinazochuliwa na serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kukabiliana na janga hilo mara baada ya kupokea ugeni kutoka Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi.
    Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa ambaye pia ni diwani wa kata ya Gongolamboto akitoa ufafanuzi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho kwa kuhusu hatua iliyofikiwa na mikakati ya manispaa ya Ilala katika kukabiliana na maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi.
    Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Jerry Silaa akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho (kulia) na Diwani wa Viti maalum Ilala Mh.Batuli Mziya (katikati) wakati wa ziara ya viongozi wa TACAIDS kata ya Gongolamboto.
    Mmoja wa wanachama wa Asasi ya Vijana ya St. Camilus inayojihusisha na utoaji wa elimu kuhusu VVU na Ukimwi kwa vijana kupitia sanaa mbalimbali Bi. Aquila Mawenya akisoma taarifa ya utendaji kazi wa asasi hiyo kwa Mwenyekiti wa wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Dkt. Fatma Mrisho alipokutana na wanachama wa Asasi hiyo Kiwalani jijini Dar es salaam.

    Mwenyekiti wa wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho (katikati) akiwa na baadhi ya wanachama Asasi ya Vijana ya St. Camilus inayojihusisha na utoaji wa elimu kuhusu VVU na Ukimwi kwa vijana kupitia sanaa mbalimbali alipowatembela eneo la Kiwalani jijini Dar es salaam.
    Baadhi ya viongozi wa manispaa ya Ilala wakiongozwa na Meya wa Manispaa hiyo Mh. Jerry Silaa (katikati) wakiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Dkt. Fatma Mrisho (wa tatu kutoka kulia) alipotembelea Kata ya Gongolamboto kuangalia hatua zilizofikiwa katika kupambana na ugonjwa huo katika ngazi ya kata.
    Picha na 10. Mwenyekiti wa wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho akikutana na vijana wa kata ya Vingunguti wa Asasi ya Watoto na Vijana –CAFLO. Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.
    Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho akizungumza na viongozi na wakazi wa kata ya Gongolamboto jijini Dar es salaam alipotembelea eneo hilo kuangalia hatua zilizofikiwa katika kupambana na ugonjwa huo katika ngazi ya kata.
    Katibu wa mtandao wa Vikoba vya watu wanaoishi na VVU (IDINEPA VICOBA) kata ya Kiwalani Bw. Shaban Mwasa Wamikole akimkabidhi risala ya kikundi hicho Mwenyekiti wa wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Dkt. Fatma Mrisho alipokutana na wanachama wa kikundi hicho katika kata ya Kiwalani jijini Dar es salaam.

    MAAMBUKIZI YA VVU JIJINI DAR ES SALAAM YAPUNGUA.
    Na. Aron Msigwa –MAELEZO.
    18/6/2014. Dar es salaam.


    Licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali za udhibiti wa maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, Jiji la Dar es salaam limefanikiwa kupunguza kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 9.8 za mwaka 2007/2008 hadi kufikia asilimia 6.9 kutokana na jitihada zilizofanywa na serikali zikiwemo za uundaji wa kamati shirikishi za mkoa kudhibiti maambukizi hayo. 


    Hayo yamebainishwa katika taarifa ya hali ya maambukizi ya VVU na Ukimwi iliyotolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam Bi. Terezia Mmbando kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho alipotembelea maeneo mbalimbali ya jiji hilo kuangalia hatua zilizofikiwa katika kupambana na ugonjwa huo.


    Akisoma taarifa hiyo leo jijini Dar es salaam Bi. Mmbando ameeleza kuwa janga la Ukimwi ni tatizo la dunia nzima na limekuwa kikwazo cha maendeleo ya jamii hapa nchini na kuongeza kuwa jitihada za kudhibiti maambukizi ya Ukimwi jijini Dar es salaam zimechukuliwa kupunguza maambukizi ikiwa ni pamoja na uanzishaji rasmi wa kamati za kuratibu na kusimamia shughuli za kudhibiti Ukimwi kuanzia ngazi ya mkoa, halmashauri, ngazi ya kata na mtaa.


    Amesema jiji la Dar es salaam linakabiliwa na changamoto ya ongezeko la kubwa la watu ikilinganishwa na mikoa mingine hali inayochangia mwingiliano wa tamaduni, shughulim mbalimbali, masuala ya kijamii,kimila na kiuchumi na kuongeza kuwa kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi 2012 idadi ya watu imefikia 4,364,54, wanaume wakiwa 2,125,786 na wanawake 2,238,755 sawa na ongezeko la asilimia 5 kwa mwaka.


    Hali ya VVU na Ukimwi mkoa wa Dar es salaam.
    Hali ya maambukizi ya Ukimwi katika jiji la Dar es salaam kwa mujibu wa matokeo ya utafiti uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kuhusu viashiria vya Ukimwi na Malaria mwaka 2011/2012 inaonesha kuwa kiwango cha maambukizi ya VVU kitaifa ni wastani wa asilimia 5.1 ambapo maambukizi kwa wanawake ni asilimia 6.2 na wanaume ni asilimia 3.8.


    Sababu za maambukizi.
    Miongoni mwa sababu zinazochangia kuendelea kuwepo kwa maambukizi mapya ya VVU katika mkoa wa Dar es salaam ni pamoja na kasi ya ukuaji wa jiji na shughuli za kibiashara hali inayosababisha mwingiliano wa watu na mahusiano ya kimapenzi pia baadhi ya wakazi kutobadili tabia licha ya kupatiwa elimu ya kujikinga na maambukizi ya ya ugonjwa huo.


    Sababu nyingine ni hali ngumu ya uchumi hususani maeneo yenye mkusanyiko mkubwa wa wakazi wa kipato cha chini,kuongezeka kwa vitendo vya ngono isiyo salama hususani maeneo yenye nyumba nyingi za kulala wageni, kumbi za starehe, madangulo na makundi yaliyo katika mazingira hatarishi ya madereva wa magari ya masafa marefu.


    Aidha, ngoma za usiku zinazokesha hasa maeneo ya pembezoni mwa jiji zinazoambatana na unywaji wa pombe kupita kiasi na uwepo wa makundi maalum ya watu wanaofanya biashara ya ngono na wale wanaotumia dawa za kulevya hali inayowafanya washindwe kutoa maamuzi sahihi ya kujikinga na VVU ni miongoni mwa sababu zinazochangia maambukizi mapya ya VVU.


    Hatua zilizochukuliwa kudhibiti maambukizi.
    Mkoa kwa kushirikiana na halmashauri za manispaa na wadau mbalimbali pamoja na mambo mengine umeendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na maambukizi ya VVU,kuhamasisha upimaji wa hiari wa VVU pia kuongeza nguvu katika mapambano ya kuzuia maabukizi kutoka mama kwenda kwa mtoto kupitia kliniki za afya ya uzazi. 


    Hatua nyingine ni utoaji wa huduma za tiba na virutubisho kwa wagonjwa, kuwahudumia watoto yatima na wale wanaoishi mazingira hatarishi pia kutoa mafunzo ya ujasiriamali na kuhamasisha uundaji wa vikundi vya ujasiriamali kwa wanaoishi na VVU ili waweze kumudu gharama za maisha na uundaji wa vikundi vya sanaa vya vijana kwa ajili ya kutoa elimu ya VVU na Ukimwi kwa vijana walio katika mazingira hatarishi ya maambukizi katika jiji la Dar es salaam.


  • June 16, 2014

  • KUWEKA SIMU MFUKONI KUNAATHIRI MBEGU ZA KIUME?SOMA HAPA



    KUWEKA SIMU MFUKONI KUNAATHIRI MBEGU ZA KIUME?SOMA HAPA
    Uchunguzi wa utafiti kutoka chuo kikuu cha Exeter nchini Uingereza, unapendekeza kuwa idadi ya mbegu za uzazi za wanaume huathiriwa kwa kuweka simu za mkononi kwenye mifuko ya suruale
    Hata hivyo ,mwana sayansi wa maswala ya uzazi na shahawa,alisema kuwa ushahidi huo bado haukuwa na uhakika wowote hivyo basi simu yake bado inaendelea kukaa mfukoni mwake.
    Uchunguzi huo uliochapishwa katika jarida la 'Environment International' ulilaumu mnunurisho wa kielectromagnetiki kuwa chanzo kikuu.
    Lilichanganua tafiti kumi tofauti kuonyesha ubora wa shahawa ikihusisha wanaume 1,492.Hii ilijumuisha kupimwa kwa shahawa zilizowekwa wazi kwa mnunurisho wa simu za rununu, kwa maabara na udadisi wa wanaume katika cliniki za uzazi
    Kiongozi wa uchunguzi huo Dkt.Fiona Mathews aliambia BBC kuwa kutokana na uchunguzi huo,moja tu ndio ulionyesha uhusiano kati ya utumizi wa simu na kudidimia kwa ubora wa shahawa.
    "Nafikiri kwa mwanamume wa makamu hakuna haja ya kuingiwa na hofu,iwapo unajua una uwezekano wa kuwa na shida ya kizazi basi itakuwa jambo la busara kutoweka simu mfukoni ,pia kugeuza mtindo wako wa kula."


    Mbegu za uzazi za wanaume zinasemekana kuathirika kutokana na simu za mkononi
    'Uchunguzi zaidi'
    Alikubali kukosolewa na wana sayansi wengine huku akiunga mkono kuwa kuna umuhimu wa kufanya uchunguzi zaidi.
    Dkt,Mathews alimaliza kwa kusema"hili ni jambo la kusisimua lakini hatusemi kwa 

     
    uhakika kuwa kila anayebeba simu mfukoni atakuwa na shida ya kizazi."
    Dkt.Allan Pacey kutoka chuo kikuu cha Sheffield anasema kuwa wazo hilo la kudidimia kwa shahawa na kuharibu "DNA"linatokana na "radio frequency" na mnunurisho wa kielectromagnetiki zinazopatikana kwenye simu na pengine joto aidha moja kwa moja kutoka kwenye simu au mnunurisho.
    Dkt huyo anayefanya uchunguzi wa shahawa bado hajashawishika akisema ushahidi huo hauna msingi na ataendelea kuweka simu mfukoni.
    Aliambia BBC,"kumekuwa na shauku kwa mda kama kuweka rununu mfukoni kunaweza changia kudidimia kwa ubora wa shahawa na nguvu za kiume kivyovyote.
    "Kumekuwa na habari zisizokuwa na msingi lakini kwa maoni yangu uchunguzi uliofanywa hadi kufika sasa haujakuwa wa kutosha kwa sababu wachunguzi aidha hawakuhifadhi shahawa vile inavyofaa ama wamedadisi matumizi ya simu kati ya wanaume bila kuzingatia mambo mengine kama mitindo yao ya maisha.
    "Tunayohitaji ni uchunguzi kufanywa ambapo utumizi wa simu unazingatiwa vile vile tabia zinazoathiri maisha yao.
    Hadi pale tutakapo tafakari hayo,nitaendelea kuweka simu yangu katika mfuko wa mkono wa kulia wa suruale yangu!"

  • June 13, 2014

  • Dawa za nywele relaxer zinazosababisha uvimbe wa kizazi kwa wanawake.


    BREAKING NEWS: Dawa za nywele relaxer zinazosababisha uvimbe wa kizazi kwa wanawake..SOMA ZAIDI HAPA!! UKIPUUZIA IMEKULA KWAKO!!

    Dawa za kulainisha nywele (relaxer) zimekuwa zinapendwa na wanawake wengi wa Afrika kwa kuwa zina uwezo wa kulainisha nywele na kumfanya apendeze na awe wa kuvutia.
    Hata hivyo, wataalamu wa afya wanadai kuwa dawa hizo zinasababisha uvimbe kwenye kizazi kutokana na kemikali za dawa hizo ambazo huingia mwilini kupitia majeraha au ngozi wakati wa kupaka.
    Daktari wa Manispaa ya Ilala, Laurent Chipata alifanya utafiti na kubaini kuwa dawa za nywele na vipodozi zina kemikali ambazo husababisha uzalishwaji wa vichocheo kwa kiasi kikubwa na kusababisha uvimbe kwenye kizazi uitwao fibroids au leimyoma.
    "Kemikali hizi hupenya kwenye ngozi na wakati mwingine hata kwa harufu tu, husababisha kuzalishwa kwa wingi wa vichocheo aina ya estrogen ambavyo huchangia kuota kwa uvimbe wa fibroids," anasema.
    Dk Chipata anasema kukua kwa uvimbe kwenye kizazi hutokea katika kipindi ambacho mama yupo kwenye uzazi yaani kabla hajakoma hedhi.
    Utafiti wa Dk Chipata ulifanywa nchini na kujumuisha wanawake wa kada tofauti tofauti wanaotumia dawa za nywele na wale wasiotumia na ukubwa wa tatizo hili ulibainika.
    "Zipo kemikali tofauti tofauti zinazosababisha uvinbe kwenye kizazi, zipo za kwenye dawa za kilimo kama DDT na za kwenye mafuta ya ngozi kama vile mercury na hydroquionone," anasema.
    Dk Chipata anasema madhara yanayopatikana katika kemikali za vipodozi ni makubwa siyo tu kwenye kizazi bali nyingine husababisha saratani au kufeli kwa figo. Anatoa mfano wa kemikali ya zebaki (mercury).
    "Dawa za nywele zina madhara si lazima zipenye kwenye ngozi baada ya mtu kupata jeraha la kuungua bali zinaweza kupenya zenyewe kwenye ngozi kutokana na mfumo wa ngozi," anasema.
    Anashauri kuwa ni vyema watu wakasoma kipodozi kimetengenezwa kwa nini kabla ya kukitumia na kuongeza kuwa ni salama zaidi kubaki na ngozi au nywele halisi badala ya kujibadilisha.
    Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekataza vipodozi vyenye kemikali kama biothionol, hexachlorophene, mercury, vinyl chloride, zirconium na bidhaa zenye aerosol, chloroquionone, steroids, methylene na chloroform.
    Utafiti mwingine uliofanywa mwaka 2012 na Dk Lauren Wise na wenzake nchini Marekani na kuchapishwa kwenye jarida la afya la nchini Marekani ulibaini kuwa vipodozi vingi vina kemikali zenye vichocheo vya estrogen ambavyo kwa kawaida huchochea kasi ya kuota kwa uvimbe kwenye kizazi cha mwanamke na wakati mwingine kwenye mji wa mimba. Kitaalamu uvimbe au vivimbe hivi hujulikana kama fibroids au myoma.
    Dk Wise anasema aliwafanyia uchunguzi wanawake wanaotumia dawa za kulainisha nywele na kuangali umri walioanza kutumia dawa hizo, mara ngapi, waliungua kiasi gani na walikaa na dawa hizo kichwani kwa kipindi gani.
    Aliwafuatilia wanawake 23,580 wanaotumia dawa za kulainisha nywele na baada ya kipindi fulani walipimwa. Kati yao, 7146 waligundulika kuwa na uvimbe kwenye kizazi baada ya kupimwa kwa mionzi na wengine kufanyiwa upasuaji.
    Kwa nini relaxer ni hatari kwa wanawake?
    Dk Wise anasema mchanganyiko ulio kenye dawa za nywele hasa zilizoandikwa "Lye Relaxer" ni sodium hydroxide wakati makopo ya dawa yaliyoandikwa "No Lye Relaxer" yana calcium hydroxide na guanidine carbonate.
    Bidhaa za kulainishwa nywele zilizoandikwa 'no lye relaxer' zinadaiwa kusababisha majeraha kwa kiasi kidogo ukilinganisha na zile zilizoandikwa "Lye Relaxer".
    Uvimbe kwenye kizazi ni nini?
    Ukuta wa nyumba ya uzazi umejengwa kwa misuli ya tishu. Kwa kawaida uvimbe huu huanza kidogo kidogo na hukua hadi kufikia ukubwa wa tikiti maji. Fibroids kubwa huweza kukua na kutanua nyumba ya uzazi na kuwa sawa na ujauzito wa miezi sita au saba.
    Mwanamke huweza kuwa na uvimbe mmoja mkubwa au vivimbe vingi ndani ya kizazi.
    Daktari Bigwa wa magonjwa ya uzazi wa Kitengo cha Upasuaji cha Chuo Kikuu Sayansi ya Tiba Muhimbili, Henry Mwakyoma anauelezea fibroids ni uvimbe ambao upo katika umbile la misuli myembamba na laini linalokua siku hadi siku.
    "Sababu inayopewa kipaumbele zaidi ni wingi wa vichocheo vya estrogen ambavyo vipo katika miili ya wanawake," anasema.
    Dk Mwakyoma anafafanua kuwa, vichocheo hivi ndivyo hufanya kazi katika mwili wa mwanamke na kumsababishia kupata siku zake za hedhi.
    "Ndiyo maana wengi wanaopata uvimbe huu, huwa ni wanawake walio katika umri mkubwa au ambao tayari wamevunja ungo, kwani ndiyo ambao huzalisha vichocheo vya estrogeni," anabainisha mtaalamu huyo.
    "Dalili hutegemeana na eneo ulipokaa uvimbe na ukubwa wake. Wengi hugundulika wakati wa kujifungua au endapo mwanamke atapata uvimbe katikati ya kizazi, basi huweza kutokwa damu kwa wingi," anasema.
    Anaongeza: "Hata hivyo, asilimia 35 hadi 50 ya wanawake wanaougua maradhi haya huonyesha dalili wakati wa kujifungua,"
    Dalili nyingine ni mwanamke kutokwa damu zake za hedhi kwa wingi na kwa siku nyingi. Damu za hedhi huweza kuwa nyingi au kidogo sana zikiambatana na maumivu makali.
    Anasema wakati mwingine mwanamke huweza kuhisi ana ujauzito kwani uvimbe huu huwa mkubwa na huchezacheza kana kwamba ni kiumbe.
    "Nina mifano hai, wapo wanawake waliowahi kuhisi wana ujauzito, wakakosa kabisa siku zao za hedhi, wakaona dalili zote za mimba na kumbe walikuwa na uvimbe wa fibroids," anasema.
    Msemaji wa TFDA, Gaudensia Simwanza anasema wamekuwa wakifanya ukaguzi mara kwa mara kuzuia uuzwaji wake.
    Isitoshe akasema: "Elimu inatolewa kwa wananchi pia ili kuwafahamisha kuhusu madhara ya vipodozi hivyo kwa sababu wanunuzi wasipokuwepo basi hata biashara haitakuwepo."
    Pamoja na hayo, adhabu hutolewa ya kuwanyang'anya na kuwapeleka mahakamani wenye maduka makubwa wakiziuza.


    CHANZO: GAZETI LA MWANANCHI


  • June 04, 2014

  • NHIF WAANZA UTARATIBU WA UCHAKUAJI WA MTU MMOJA MMOJA


    NHIF WAANZA UTARATIBU WA UCHAKUAJI WA MTU MMOJA MMOJA
    MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya  (NHIF) umeazimia kuongeza wanachama wake ambao kwa sasa ni asilimia 7.4 ya Wananchi wote kwa kuvisajili vikundi mbalimbali vya wajasiriamali na ushirika katika huduma za Mfuko kwa kupitia uchangiaji wa mtu mmoja mmoja.
    Hayo yamo katika hotuba ya Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii iliyosomwa Bungeni jana.
    Waziri wa wizara hiyo Dk Seif Rashid alisema katika utaratibu huo, uongozi wa vikundi ndiyo utakuwa wadhamini na pia ndiyo utakaokuwa wakala wa Mfuko katika ukusanyaji wa michango na ufuatiliaji wa upatikanaji wa huduma.
     Mkakati huoumelenga kuongeza wigo wa wanufaika wa huduma za bima ya afya nchini kufikia asilimia 30 ifikapo mwaka 2015. Kwa sasa huduma hiyo imefikia asilimia 19.2.
     Vilevile, alisema Mfuko utafanya tathmini ya nne ya Mfuko ili kuangalia uhai wa Mfuko na huduma zake kwa wanachama.
    Akizungumzia  utaratibu wa kugharimia huduma za afya kwa kuchangia Mfuko wa Afya wa Jamii (CHF) kwa ajili ya sekta isiyo rasmi na wananchi waishio vijijini, Waziri huyo wa Afya alisema hadi kufikia mwezi Machi, 2013 Watanzania 4,010,844 sawa na asilimia 9.2 walikuwa wamejiunga na Mfuko huo.
    Aidha Dk Rashid alisema kutokana na tathmini iliyofanywa, Mfuko wa Afya wa Jamii kwa sehemu za mjini umeanza kutumika katika mkoa wa Dar es Salaam kwa kuhusisha vikundi vya uzalishaji.
    Alisema katika hotuba yake kwamba katika mwaka 2014/15 utaratibu huo unaojulikana kama Tiba kwa Kadi (TIKA) unatarajiwa kuenezwa katika mikoa ya Mwanza, Singida, Ruvuma, Pwani, Tanga, Lindi na Kilimanjaro.
    "Naomba nichukue nafasi hii kuwashauri Waheshimiwa Wabunge wote kujiunga na Mfuko huo ili kuwa mfano na kutoa elimu ya Mfuko huo katika maeneo yenu ili wananchi wengi waweze kujiunga. Mimi binafsi nimejiunga na Mfuko huu na nimeona faida zake hivyo nawaomba wananchi wote nchini wajiunge na Mfuko huo" alisema Waziri Rashid.
    Aidha alisema Wizara imekamilisha na kuzindua Mpango Mkakati wa Matumizi ya TEHAMA katika sekta ya afya wa mwaka 2013 - 2018, ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Afya ya mwaka 2007, inayoelekeza matumizi ya mfumo endelevu wa habari na mawasiliano katika shughuli za sekta ya afya.
     Akifafanua zaidi amesema Wizara yake pia imeboresha huduma za tiba kwa njia ya mtandao - telemedicine, na kuwa hadi sasa huduma hiyo inajumuisha hospitali ya rufaa ya kanda Mbeya, Temeke, Bagamoyo, Mwananyamala, Amana, Tumbi na Hospitali ya Rufaa ya Taifa ya Muhimbili.
    Katika mwaka huu wa fedha Wizara itaunganisha Hospitali za Rufaa za Kanda (Bugando na KCMC), na Hospitali maalumu (Mirembe, Ocean Road na MOI) katika mfumo wa telemedicine ili kuboresha huduma za ushauri na tiba katika mtandao na kupunguza rufaa zisizo za lazima.
    Akizungumzia vyanzo  vya kugharamia huduma za afya, Dk Rashid alisema Bima za afya imekuwa moja ya vyanzo muhimu sana katika vituo vya kutolea huduma za afya na kupunguza pengo la mahitaji ya raslimali fedha kwa kiwango kikubwa.
    Alisema kutokana na Ripoti ya Mapitio ya Matumizi ya Fedha za Umma (Public Expenditure Review – PER, 2012) inaonesha kwamba vyanzo mbadala vinachangia wastani wa asilimia 5 ya mapato yote ya Halmashauri kwa sekta ya afya.
    " Hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2014 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya uliwalipa watoa huduma za matibabu kiasi cha Sh. bilioni 77.7. " alisema na kuongeza kuwa:Mfuko umeanza kutekeleza utaratibu wa kuwaunganisha watoa huduma katika mtandao wa kompyuta ili wawe wanaandaa na kuwasilisha madai kwa njia ya kielektroniki.
    Alisema hatua hiyo imekusuduia kupunguza muda wa malipo na kuharakisha utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa e-Health ambao Wizara iliuzindua Oktoba mwaka jana.
    Nayo Kamati ya Bunge ya afya imesema ipo haja ya Huduma za bima ya afya ziwafikie wananchi wote ikijumuisha wazee, watoto, watu wenye ulemavu, yatima, wajawazito na wasio na kipato kama haki yao ya msingi.
    Aidha imeitaka Serikali ibuni njia mbadala ya kupata fedha kutekeleza mradi wa ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Kanda ya Kusini inayotakiwa kuejengwa Mtwara.
    Kuhusu ujenzi na karabati wa vituo vya kutoa huduma , kamati hiyo ya kudumu ya bunge imetaka kuandaliwa kwa mikakati maalumu ili kupunguza utegemezi kwa kushirikisha wadau wa ndani
    Nayo kambi ya upinzani katika hotuba yake imetaka Mifuko inayogharamia huduma za Afya (NHIF, CHF/TIKA, CBHI, NSSF-SHIB) iwekewe utaratibu wa kufanyakazi kwa pamoja.
    Aidha wametaka mapendekezo ya Mfumo wa ugharamiaji huduma za afya kwa wote yawasilishwe kwa Wadau wakiwemo waheshimiwa Wabunge na waelimishwe kuhusu dhana hiyo.
    Usimamizi wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) uimarishwe hususani katika eneo la fedha zinazochangwa na wananchi.


  • Copyright @ 2013 Michapo | Kisiwa cha Habari.