Na Insp. Deodatus Kazinja,PHQ
Aliyewahi kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza Mzee Josephat Mwingira aliyefariki tarehe 09 Juni, 2014 na kuzikwa tarehe 12 Juni,2014 katika Makaburi ya Kunduchi Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es salaam kwa heshima zote za kijeshi.
Marehemu Mwingira aliajiriwa katika Jeshi la Magereza tarehe 11 January 1956 ambapo alianzia kazi katika Gereza Kuu Butimba la Jijini Mwanza na maeneo mengine mengi nchini hadi alipo staafu kwa mujibu wa sheria tarehe 01 Julai, 1990 akiwa amelitumikia Jeshi la Magereza kwa miaka 33.
Hayati Mwingira mbali na kuwa kiongozi katika Jeshi la Magereza lakini pia alikuwa kada maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na alishika nyadhifa kadhaa enzi za siasa majeshi.
Kamishana Jenerali wa Jeshi la Magereza kwa niaba ya watumishi wote wa Jeshi la Magereza anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu mzito.
Picha zote na Insp. Deodatus Kazinja, Makao Makuu ya Magereza
0 comments:
Post a Comment