August 26, 2015

UKAWA WATAKA MAGUFULI AONGEZEWE ULINZI



UKAWA WATAKA MAGUFULI AONGEZEWE ULINZI

East Africa Radio
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar, Bw. Salum Mwalimu, amewataka CCM, kumwongezea ulinzi mgombea urais wao wa Jamhuriya Muungano, Dkt. John Magufuli ili asijiunge UKAWA. Alisema hivi sasa viongozi wa CCM wameimarisha ulinzi kwa makada wao wote maarufu ili wasijiunge UKAWA. "CCM wamwongezee ulinzi Dkt. Magufuli, wakimwachia dakika tano watasikia naye amejiunga UKAWA." Bw. Mwalimu aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika juzi Kibandamaiti visiwani Zanzibar. source: MAJIRA


No comments:

Post a Comment